Swali 64: Ni kina nani walikuwa wajumbe wa mwaka huu waliofuatana katika mpangilio wa matukio?
Jibu: Ujumbe wa Tamiym. Kuhusiana na hilo kukateremshwa:
إِنَّ الَّذِينَ يُنَادُونَكَ مِن وَرَاءِ الْحُجُرَاتِ أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ
”Hakika wale wanaokuwita nyuma ya vyumba wengi wao hawatii akilini.”[1]
Ujumbe wa ´Abdul-Qays. Walifika kabla ya Ufunguzi.
Ujumbe wa Banuu Haniyfah. Miongoni mwao alikuwepo Musaylimah Mwongo.
Ujumbe wa Najraan. Kuliteremshwa juu yao zile Aayah 83 za mwanzo wa Suurah ”Aal ´Imraan”.
Ujumbe wa Banuu ´Aamir.
Ujumbe wa Dhwimaam bin Tha´labah.
Ujumbe wa Tway´ pamoja na Zayd bin al-Khayl.
Ujumbe wa ´Adiy bin Haatim.
Ujumbe wa Daws huko Khaybar. Uliongozwa na at-Twufayl. Alifika kabla ya Ufunguzi na akaingia katika Uislamu.
Ujumbe wa Ash´ariyyuun pamoja na wale Wahajiri waliofanya Hijrah mara mbili.
Ujumbe wa Farwah bin Musayk al-Muraadiy kwa niaba ya watu wake.
Ujumbe wa Azd.
Ujumbe wa al-Ash´ath bin Qays al-Kindiy.
Mjumbe wa wafalme wa Himyar ambaye alitangaza Uislamu wa watu wake pamoja na barua ya Dhuu Yazan. Kwa hiyo Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) aliwarudishia barua inayotambulika sana ya ´Amr bin Hazm.
Ujumbe wa Jariyr al-Bajaliy.
Ujumbe wa Waa-il bin Hujr.
Ujumbe wa Abu Raziyn al-´Uqayliy.
Ujumbe wa Sudaa´.
Ujumbe wa al-Haarith al-Bakriy.
Ujumbe wa Ashjaa´.
Ujumbe wa Farwah al-Judhaamiy. Warumi wakamuua.
Ujumbe wa Tamiym bin Aws ad-Daariy.
Ujumbe wa Fizaarah.
Ujumbe wa Asad.
Ujumbe wa Banuu ´Abs. Ulikuwa kabla ya Ufunguzi na kabla ya mkataba wa Hudaybiyah.
Ujumbe wa Banuu Murrah.
Ujumbe wa Banuu Tha´labah huko Ji´irraanah.
Ujumbe wa Banuul-Haarith katika mwaka wa 10 wakati wa hijjah ya kuaga.
Ujumbe wa Banuu Kilaab.
Ujumbe wa Banuu ´Aqiyl Ka´b.
Ujumbe wa Banuu Qushayr bin Ka´b.
Ujumbe wa Kinaanah.
Ujumbe wa Baahilah.
Ujumbe wa Banuu Sulaym kabla ya Ufunguzi ambao walioushuhudia.
Ujumbe wa Hilaal bin ´Aamir.
Ujumbe wa Banuu Bakr.
Ujumbe wa Taghlab.
Ujumbe wa Tujiyb kutokea Yemen.
Ujumbe wa Khawlah mwaka wa 10.
Ujumbe wa Ju´fiy.
Ujumbe wa Azd.
Ujumbe wa Banuu Sa´d Hudhaym.
Ujumbe wa Bahraa´.
Ujumbe wa Udhrah.
Ujumbe wa Baliy. Miongoni mwao walikuwepo waulizaji kuhusu kilichookotwa.
Ujumbe wa Ghassaan mwaka wa 10.
Ujumbe wa Ghaamid mwaka wa 10.
Ujumbe wa Nakha´iy. Huu ndio ulikuwa ujumbe wa mwisho na ulitokea Muharram mwaka wa 11.
[1] 49:04
- Mhusika: ´Allaamah Haafidhw bin Ahmad al-Hakamiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Amaaliy fiys-Siyrah an-Nabawiyyah, uk. 126-131
- Imechapishwa: 30/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)