Shaykh (Rahimahu Allaah) amesema kwamba imamu na anayeswali peke yake wanatakiwa kusema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”,
na si maamuma, jambo ambalo ndio sahihi. Hilo ni kutokana na maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Hakika imamu amewekwa ili afuatwe… ” na ndani yake imekuja: “Anaposema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”,
semeni:
ربنا ولك الحمد
”Mola wetu, himdi zote ni Zako.”
Ameipokea al-Bukhaariy (732–734) kupitia kwa Anas na Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhumaa). Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Hadiyth hizo mbili: ”Semeni:
ربنا ولك الحمد
”Mola wetu, himdi zote ni Zako.”
Hakusema: ”Semeni:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”
Baadhi ya wanazuoni wameona kuwa maamuma pia anatakiwa kusema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”
hali ya kujengea hoja ujumla wa maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Hadiyth ya Maalik bin al-Huwayrith:
“Swalini kama mnavyoniona ninaswali.”
Ameipokea al-Bukhaariy (631).
Njia ya hoja ni kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”
Kwa hivyo mamuma pia wanatakiwa kusema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”
Kuhusu Hadiyth inayosema: “Anaposema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”,
semeni:
ربنا ولك الحمد
”Mola wetu, himdi zote ni Zako.”
ni yenye kufungamanishwa na Hadiyth isemayo:
“Swalini kama mnavyoniona ninaswali.”
Hilo ni kama mfano wa maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mnaposikia adhaana basi semeni kama anavyosema muadhini.”
Ameipokea al-Bukhaariy (611) na Muslim (383) kupitia kwa Abu Sa’iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ‘anh). Hadiyth hiyo imefungamanishwa na Hadiyth isemayo:
حي على الصلاة، حي على الفلاح
”Njooni katika swalah, njooni katika mafanikio.”
Mwitikiaji anatakiwa kusema:
لا حول ولا قوّة إلاّ بالله
”Hapana kutikisika wala nguvu isipokuwa kwa msaada wa Allaah.”
Hivo ndivo imekuja katika ”as-Swahiyh” ya Muslim (385) kupitia kwa ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anh).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbaad
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 91-93
- Imechapishwa: 06/07/2026
Shaykh (Rahimahu Allaah) amesema kwamba imamu na anayeswali peke yake wanatakiwa kusema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”,
na si maamuma, jambo ambalo ndio sahihi. Hilo ni kutokana na maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Hakika imamu amewekwa ili afuatwe… ” na ndani yake imekuja: “Anaposema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”,
semeni:
ربنا ولك الحمد
”Mola wetu, himdi zote ni Zako.”
Ameipokea al-Bukhaariy (732–734) kupitia kwa Anas na Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhumaa). Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Hadiyth hizo mbili: ”Semeni:
ربنا ولك الحمد
”Mola wetu, himdi zote ni Zako.”
Hakusema: ”Semeni:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”
Baadhi ya wanazuoni wameona kuwa maamuma pia anatakiwa kusema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”
hali ya kujengea hoja ujumla wa maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Hadiyth ya Maalik bin al-Huwayrith:
“Swalini kama mnavyoniona ninaswali.”
Ameipokea al-Bukhaariy (631).
Njia ya hoja ni kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”
Kwa hivyo mamuma pia wanatakiwa kusema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”
Kuhusu Hadiyth inayosema: “Anaposema:
سمع الله لمن حمده
”Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”,
semeni:
ربنا ولك الحمد
”Mola wetu, himdi zote ni Zako.”
ni yenye kufungamanishwa na Hadiyth isemayo:
“Swalini kama mnavyoniona ninaswali.”
Hilo ni kama mfano wa maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mnaposikia adhaana basi semeni kama anavyosema muadhini.”
Ameipokea al-Bukhaariy (611) na Muslim (383) kupitia kwa Abu Sa’iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ‘anh). Hadiyth hiyo imefungamanishwa na Hadiyth isemayo:
حي على الصلاة، حي على الفلاح
”Njooni katika swalah, njooni katika mafanikio.”
Mwitikiaji anatakiwa kusema:
لا حول ولا قوّة إلاّ بالله
”Hapana kutikisika wala nguvu isipokuwa kwa msaada wa Allaah.”
Hivo ndivo imekuja katika ”as-Swahiyh” ya Muslim (385) kupitia kwa ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anh).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbaad
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 91-93
Imechapishwa: 06/07/2026
https://firqatunnajia.com/64-maamuma-aitikie-kama-imamu/