Swali: Allaah (Ta´ala) amesema:
وَوَيْلٌ لِّلْمُشْرِكِينَ الَّذِينَ لَا يُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَهُم بِالْآخِرَةِ هُمْ كَافِرُونَ
“Na ole kwa washirikina. Ambao hawatoi zakaah nao ni wenye kuikanusha Aakhirah.”[1]
Nini makusudio yake?
Jibu: Inaweza kuwa na maana mbili:
1 – Makusudio ya zakaah ni utakaso wa nafsi, kwa maana ya kuisafisha kutokana na shirki. Amesema (Ta´ala) amesema:
قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّاهَا
“Hakika amefaulu yule aliyeitakasa.”[2]
Kutokana na tafsiri hiyo Aayah inawakusudia washirikina wasiojitakasa kutokana na shirki na njia zake.
2 – Zakaah ya aina ya kujitolea mali. Kwa hiyo kule kujizuia kwao kutoa zakaah inakuwa ni moja katika sifa zao. Ingawa watatoa zakaah au wakafanya aina nyingine ya ´ibaadah basi yasingekubaliwa kutoka kwao kutokamana na shirki yao.
[1] 41:6-7
[2] 91:9
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (18/15-16)
- Imechapishwa: 05/07/2026
Swali: Allaah (Ta´ala) amesema:
وَوَيْلٌ لِّلْمُشْرِكِينَ الَّذِينَ لَا يُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَهُم بِالْآخِرَةِ هُمْ كَافِرُونَ
“Na ole kwa washirikina. Ambao hawatoi zakaah nao ni wenye kuikanusha Aakhirah.”[1]
Nini makusudio yake?
Jibu: Inaweza kuwa na maana mbili:
1 – Makusudio ya zakaah ni utakaso wa nafsi, kwa maana ya kuisafisha kutokana na shirki. Amesema (Ta´ala) amesema:
قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّاهَا
“Hakika amefaulu yule aliyeitakasa.”[2]
Kutokana na tafsiri hiyo Aayah inawakusudia washirikina wasiojitakasa kutokana na shirki na njia zake.
2 – Zakaah ya aina ya kujitolea mali. Kwa hiyo kule kujizuia kwao kutoa zakaah inakuwa ni moja katika sifa zao. Ingawa watatoa zakaah au wakafanya aina nyingine ya ´ibaadah basi yasingekubaliwa kutoka kwao kutokamana na shirki yao.
[1] 41:6-7
[2] 91:9
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (18/15-16)
Imechapishwa: 05/07/2026
https://firqatunnajia.com/zakaah-ya-washirikina/