Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:

96 – Kaburi ima ni bustani miongoni mwa mabustani ya Peponi au ni shimo miongoni mwa mashimo ya Moto.

MAELEZO

Hii ni sehemu ya Hadiyth aliyoipokea at-Tirmidhiy iliyosimuliwa na Abu Sa´iyd, kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Cheni yake ya wapokezi ni dhaifu. Sehemu yake ya mwanzo ameipokea Abu Ya´laa. Katika cheni yake ya wapokezi kuna Darraaj, kama ilivyo katika ”al-Majmaa´-uz-Zawaaid”[1], ambaye anasimulia Hadiyth zinazopingana na zilizo Swahiyh.

[1] Tazama ”Majma´-uz-Zawaa’id” (3/55).

  • Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah – Sharh wa Ta´liyq, uk. 85
  • Imechapishwa: 14/10/2024