3- Mwenye kuuliwa kwa kusimamishiwa adhabu miongoni mwa adhabu za Allaah. Hilo ni kutokana na Hadiyth ya ´Imraan bin Huswayn:
“Kuna mwanamke mmoja katika kabila la Juhaynah alimjia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiwa na ujauzito wa uzinzi ambapo akasema: “Ee Mtume wa Allaah! Nimewajibikiwa na adhabu. Nitekelezee nayo!” Mtume Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwita walii wake akamwambia: “Mtendee wema. Akishazaa niletee naye. Mtume Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwamrisha azifunge vizuri nguo zake kisha akaamrisha apigwe mawe. Halafu baadaye akamswalia. ´Umar akasema kumwambia: “Je, hivi kweli unamswalia ilihali amezini?” Akasema: “Hakika ametubu tawbah ambayo ingegawanywa kati ya watu sabini wa al-Madiynah basi ingeliwaenea. Hivi kweli ipo tawbah bora kuliko yeye mwenyewe kujileta kwa Allaah (Ta´ala)?”
Ameipokea Muslim (05/121), Abu Daawuud (02/233), an-Nasaa´iy (01/278), at-Tirmidhiy (02/325) ambaye ameisahihisha. Pia ameipokea ad-Daarimiy (02/180), al-Bayhaqiy (04/18, 19) na Ibn Maajah (02/116,117) kwa mukhtasari.
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz wa Bid´ahaa, uk. 108
- Imechapishwa: 16/07/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket