Qur-aan sio mafumbo, kama wanavyosema Jahmiyyah na Mu´tazilah. Wanasema ni maneno ya Allaah, lakini hata hivyo yananasibishwa kwa Allaah kwa njia ya mafumbo kwa kuwa Allaah ndiye ameyaumba. Hivyo wanadai kuyanasibisha kwa Allaah ni kunasibisha kiumbe kwa Mola Wake. Wamesema uwongo kwa sababu kuna aina mbili ya unasibishaji:
1 – Kuegemeza maana kwa Allaah, kama vile maneno. Pindi maana inanasibishwa kwa Allaah ni kunasibisha sifa kwa Mwenye kusifika nayo. Maneno, usikizi, uoni, uwezo na matakwa ni kuegemeza sifa kwa mwenye kusifika nazo, kwa sababu maana hizi haziwezi kusimama peke yake bali zinakuwa kwa yule mwenye kusifika nazo.
2 – Kuegemeza vitu, kama vile nyumba ya Allaah, ngamia wa Allaah na mja wa Allaah. Katika hali hii ni uegemezaji wa viumbe kwa Muumba Wake kwa njia ya utukufu.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 68-69
- Imechapishwa: 11/01/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)