10 – ´Abdullaah bin Muhammad bin ´Aqiyl amesema:
” ´Aliy bin al-Husayn alinituma kwa ar-Rubayyi´ bint Mu´awwidh kumuuliza juu ya wudhuu´ wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kwa sababu alikuwa akitawadha kwake. Nilipomwendea akachukua chombo na kusema: ”Nilikuwa nikifanya namna hii pindi ninapomletea Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) maji kwa ajili ya kutawadha.”[1]
[1] al-Humaydiy katika “al-Musnad”, at-Twabaraaniy katika “al-Mu´jam al-Kabiyr” na wengineo. Cheni yake ya wapokezi ni nzuri licha ya makinzano yaliyopo juu ya ´Abdullaah bin Muhammad bin ´Aqiyl, kama alivosema Ibn-ul-Qattwaan.
Nimetaja upokezi mfano wake katika ”Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” na humo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia mwanamke huyo:
”Nimiminie maji.”
Kwa at-Twabaraaniy imekuja:
”Nimiminie maji juu yangu.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
”Nilikuwa nikimimina maji kwenye mikono yake mara tatu.”
Kwa maana hiyo inaweza kutajwa katika kipengele cha kabla yake.
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Jilbaab-ul-Mar-ah al-Muslimah, uk. 101
- Imechapishwa: 27/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)