16 – Imependekezwa kwa mwanamke kutembelea msikiti wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa ajili ya kuswali na kuomba du´aa ndani yake. Lakini haijuzu kwake kutembelea kaburi la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa sababu amekatazwa kutembelea makaburi. Shaykh Muhammad bin Ibrahiym Aalush-Shaykh (Rahimahu Allaah), ambaye alikuwa Muftiy wa Saudi Arabia, amesema katika “Majmuu´-ul-Fatawaa”:
“Maoni sahihi katika masuala haya ni kwamba mwanamke amekatazwa kulitembelea kaburi lake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa sababu ya maambo mawili:
1 – Ueneaji wa dalili na makatazo yakitajwa kwa ujumla basi haijuzu kwa yeyote kuyafanya maalum isipokuwa kwa dalili.
2 – Jengine ni kwamba sababu imepatikana hapa.”[1]
Shaykh ´Abdul-´Aziyz bin Baaz (Hafidhwahu Allaah) amesema katika “al-Mansik” yake, wakati alipotaja kuhusu kulitembelea kaburi lake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa yule aliyetembelea msikiti wake mtukufu, akasema:
“Matembezi haya ya kaburi lake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kwa yule aliyetembelea msikiti wake mtukufu; kisha akasema: “Matembezi haya yamesuniwa kwa wanaume peke yao. Ama wanawake haifai kwao kutembelea kaburi lolote, kama ilivyothibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba amewalaani wanawake wenye kuyatembelea makaburi na wale wenye kuyafanya ni pahali pa kuswalia na wenye kuyatia mataa. Ama kukusudia al-Madiynah kwa ajili ya kuswali ndani ya msikiti wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kuomba du´aa ndani yake na mfano wa hayo ambayo yamesuniwa pia katika misikiti mingine ni jambo limesuniwa kwa wote.”
[1] (03/239).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 96
- Imechapishwa: 18/11/2019
16 – Imependekezwa kwa mwanamke kutembelea msikiti wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa ajili ya kuswali na kuomba du´aa ndani yake. Lakini haijuzu kwake kutembelea kaburi la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa sababu amekatazwa kutembelea makaburi. Shaykh Muhammad bin Ibrahiym Aalush-Shaykh (Rahimahu Allaah), ambaye alikuwa Muftiy wa Saudi Arabia, amesema katika “Majmuu´-ul-Fatawaa”:
“Maoni sahihi katika masuala haya ni kwamba mwanamke amekatazwa kulitembelea kaburi lake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa sababu ya maambo mawili:
1 – Ueneaji wa dalili na makatazo yakitajwa kwa ujumla basi haijuzu kwa yeyote kuyafanya maalum isipokuwa kwa dalili.
2 – Jengine ni kwamba sababu imepatikana hapa.”[1]
Shaykh ´Abdul-´Aziyz bin Baaz (Hafidhwahu Allaah) amesema katika “al-Mansik” yake, wakati alipotaja kuhusu kulitembelea kaburi lake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa yule aliyetembelea msikiti wake mtukufu, akasema:
“Matembezi haya ya kaburi lake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kwa yule aliyetembelea msikiti wake mtukufu; kisha akasema: “Matembezi haya yamesuniwa kwa wanaume peke yao. Ama wanawake haifai kwao kutembelea kaburi lolote, kama ilivyothibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba amewalaani wanawake wenye kuyatembelea makaburi na wale wenye kuyafanya ni pahali pa kuswalia na wenye kuyatia mataa. Ama kukusudia al-Madiynah kwa ajili ya kuswali ndani ya msikiti wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kuomba du´aa ndani yake na mfano wa hayo ambayo yamesuniwa pia katika misikiti mingine ni jambo limesuniwa kwa wote.”
[1] (03/239).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 96
Imechapishwa: 18/11/2019
https://firqatunnajia.com/49-makatazo-ya-mwanamke-kuyatembelea-makaburi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)