Swali 49: Baadhi wamesema kuwa haijuzu kusimamisha swalah ya mkusanyiko ya pili msikitini baada ya kumalizika mkusanyiko wa waswaliji. Je, kitu hiki kina msingi? Ni yepi ya sawa?
Jibu: Maneno haya si sahihi na wala hayana msingi wowote katika Shari´ah takasifu kutokana na ninavojua. Bali Sunnah Swahiyh inajulisha kinyume chake. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swalah ya mkusanyiko ni bora kuliko swalah ya anayeswali peke yake kwa ngazi ishirini na saba.”
Amesema tena (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swalah ya mwanamme na mwanamme mwingine ni takasifu zaidi kuliko swalah yake mwenyewe.”
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pindi alipomuona bwana mmoja ameingia msikitini baada ya watu kumaliza kuswali:
”Ni nani atakayemtendea wema huyu akaswali pamoja naye”?
Lakini haijuzu kwa muislamu kujichelewesha na swalah ya mkusanyiko. Bali ni lazima kwake kuharakisha wakati anaposikia adhaana.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 55
- Imechapishwa: 05/09/2022
Swali 49: Baadhi wamesema kuwa haijuzu kusimamisha swalah ya mkusanyiko ya pili msikitini baada ya kumalizika mkusanyiko wa waswaliji. Je, kitu hiki kina msingi? Ni yepi ya sawa?
Jibu: Maneno haya si sahihi na wala hayana msingi wowote katika Shari´ah takasifu kutokana na ninavojua. Bali Sunnah Swahiyh inajulisha kinyume chake. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swalah ya mkusanyiko ni bora kuliko swalah ya anayeswali peke yake kwa ngazi ishirini na saba.”
Amesema tena (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swalah ya mwanamme na mwanamme mwingine ni takasifu zaidi kuliko swalah yake mwenyewe.”
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pindi alipomuona bwana mmoja ameingia msikitini baada ya watu kumaliza kuswali:
”Ni nani atakayemtendea wema huyu akaswali pamoja naye”?
Lakini haijuzu kwa muislamu kujichelewesha na swalah ya mkusanyiko. Bali ni lazima kwake kuharakisha wakati anaposikia adhaana.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 55
Imechapishwa: 05/09/2022
https://firqatunnajia.com/49-kuswali-swalah-ya-mkusanyiko-ya-pili-baada-ya-kumalizika-ya-kwanza/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)