Kuhusu mbingu na ardhi vimekwishatoweka, kwa sababu wakazi wake ima wameingia Peponi au Motoni. Ama ´Arshi haitoteketea wala kuondoka, kwa sababu ndio paa la Peponi. Vilevile Allaah yuko juu yake, na kwa ajili hiyo kamwe haitoangamia wala kuteketea.
Kuhusu maneno Yake (Ta´ala):
وكُلُّ شَيْءٍ هَالِكٌ إِلَّا وَجْهَهُ
“Kila kitu ni chenye kuangamia isipokuwa uso Wake.”[1]
Ni pale ambapo Allaah alipoteremsha:
كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ
”Kila aliyekuwa humo [mbinguni na ardhini] atatoweka.”[2]
ambapo Malaika wakajiuliza watu wamekwishakufa na wao wenyewe walikuwa wakitamani kubaki. Ndipo Allaah (´Azza wa Jall) akateremsha Aayah ambayo akakhabarisha kuhusu wakazi wa Peponi na wakazi wa Motoni kwamba watakufa, nayo ni:
وكُلُّ شَيْءٍ هَالِكٌ
“Kila kitu ni chenye kuangamia…”[3]
Bi maana kila chenye kuishi kitakufa.
إِلَّا وَجْهَهُ
“… isipokuwa uso Wake.”
Yeye yuhai na hatokufa. Hapo ndipo na wao wakayakinisha kwamba watakufa[4].
[1] 28:88
[2] 55:26
[3] 28:88
[4] Ibn ´Aqiyl al-Hanbaliy amesema:
”Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) ameandika kitabu kinachoitwa ”ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah waz-Zanaadiqah wal-Qadariyyah.” (al-Aadaab ash-Shar´iyyah (1/274))
Ibn Taymiyyah amesema:
”Kama alivosema Imaam Ahmad katika kitabu chake ”ar-Radd ´alaaz-Zanaadiqah wal-Jahmiyyah.” (Tafsiyr Suurat-il-Ikhlaasw, uk. 239)
Ibn Kathiyr amesema:
”… na hivo ndivo alivosema Ahmad bin Hanbal katika kitabu ”ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah” (Tafsiyr al-Qur-aan al-´Adhwiym (3/304))
Ibn Hajar al-´Asqalaaniy amesema:
”Amesema waziwazi Ahmad katika kitabu “ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah.” (Fath-ul-Baariy (13/598))
- Muhusika: Imaam Ahmad bin Hanbal (afk. 241)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah waz-Zanaadiqah, uk. 170
- Imechapishwa: 05/05/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)