Nabii ni yule ambaye Allaah anamfunulia Shari´ah na asimwamrishe kuifikisha. Mtume ni yule ambaye Allaah anamfunulia Shari´ah na pia akamwamrisha kuifikisha. Haya ndio maoni yaliyotangaa zaidi kuhusu tofauti kati ya Mtume na Nabii. Mtume ni yule ambaye ameamrishwa kufikisha. Maana yake ni kwamba ameamrishwa kuwalazimisha watu ujumbe na kupambana nao kwa ajili ya jambo hilo.
Vivyo hivyo Nabii anafunuliwa na anawalingania watu kwa Allaah (´Azza wa Jall), lakini anawafata Manabii wengine waliomtangulia, kupita juu ya njia yao na hapwekeki na Shari´ah yake maalum. Ni kama mfano wa Manabii wa wana wa israaiyl; walikuja na kulingania katika Tawraat ambayo Allaah aliiteremsha kwa Muusa (´alayhis-Salaam).
Mtunzi wa kitabu amesema:
“…na Mtume Wake aliyeridhiwa.”
Maana yake ni kwamba alikuwa ameteuliwa, amechaguliwa na ameridhiwa, kwa msemo mwingine Allaah amemridhia (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 60
- Imechapishwa: 06/12/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)
Related
08. Tofauti kati ya Mitume na Manabii
Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema: 28 - Anamwongoza amtakaye. Analinda na kuafu kutokana na fadhilah. Anapotosha, anakosesha nusura na kujaribu kwa uadilifu. 29 - Wote wanaendeshwa na matakwa ya Allaah, baina ya fadhilah Zake na uadilifu Wake. 30 - Ametakasika kutokamana na wapinzani na washirika. 31 – Hakuna yeyote…
In "Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah – al-Albaaniy"
146. Hukumu ya wanaomkubali Mtume lakini wakadai kwamba ametumwa kwa waarabu pekee
Atakayedai kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametumwa kwa waarabu peke yao - kama wanavyosema kundi katika manaswara – amemkufuru Allaah (´Azza wa Jall). Miongoni mwa manaswara wako wanaokubali kwamba Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Mtume kutoka kwa Allaah, lakini hata hivyo ujumbe wake ni kwa waarabu…
In "Sharh Nawaaqidh-il-Islaam - al-Fawzaan"
124. Namna Mtume (صلى الله عليه وسلم) alivyopewa utume
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema: Alipewa utume kwa “al-Muddaththir”. Mji wake ni Makkah. Allaah Amemtuma ili kutahadharisha shirki na kulingania katika Tawhiyd. Dalili ni Kauli Yake (Ta´ala): يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ قُمْ فَأَنذِرْ وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ وَالرُّجْزَ فَاهْجُرْ وَلَا تَمْنُن تَسْتَكْثِرُ وَلِرَبِّكَ فَاصْبِرْ ”Ee uliyejigubika! Simama na uonye!…
In "Sharh Thalaathat-il-Usuwl – al-Fawzaan"