Swali 46: Ni kipi kilichosuniwa kwa ambaye amekuja amechelewa akimkuta imamu yuko katika Rukuu´? Hukumu ya kuwahi Rak´ah ni sharti awahi kusema:
سبحان ربي العظيم
“Ametakasika Mola wangu aliyetukuka.”
kabla ya imamu kuinuka?
Jibu: Maamuma akimuwahi imamu hali ya kurukuu Rak´ah hiyo imesihi ijapo hakuwahi kuleta Tasbiyh isipokuwa baada ya imamu kuinuka. Hayo ni kutokana na kuenea kwa maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Atakayewahi Rak´ah ya swalah, basi ameiwahi swalah.”
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Ni jambo linalotambulika kuwa Rak´ah inawahiwa kwa kuwahi Rukuu´. Hilo ni kutokana na yale aliyopokea al-Bukhaariy kutoka kwa Abu Bakrah ath-Thaqafiy (Radhiya Allaahu ´anh):
“Ya kwamba siku moja alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamkuta amerukuu ambapo na yeye akarukuu nje ya safu. Kisha akajiunga ndani ya safu. Wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipotoa salamu akamwambia:
“Allaah akuzidishie pupa na usirudie.”
Hakumwamrisha kulipa Rak´ah nyingine. Alichomkataza ni kujiunga na swalah nje ya safu. Kwa hivyo ni lazima kwa ambaye amekuja kuchelewa asifanye haraka ya Rukuu´ mpaka kwanza afike katika safu.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 53-54
- Imechapishwa: 01/09/2022
Swali 46: Ni kipi kilichosuniwa kwa ambaye amekuja amechelewa akimkuta imamu yuko katika Rukuu´? Hukumu ya kuwahi Rak´ah ni sharti awahi kusema:
سبحان ربي العظيم
“Ametakasika Mola wangu aliyetukuka.”
kabla ya imamu kuinuka?
Jibu: Maamuma akimuwahi imamu hali ya kurukuu Rak´ah hiyo imesihi ijapo hakuwahi kuleta Tasbiyh isipokuwa baada ya imamu kuinuka. Hayo ni kutokana na kuenea kwa maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Atakayewahi Rak´ah ya swalah, basi ameiwahi swalah.”
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Ni jambo linalotambulika kuwa Rak´ah inawahiwa kwa kuwahi Rukuu´. Hilo ni kutokana na yale aliyopokea al-Bukhaariy kutoka kwa Abu Bakrah ath-Thaqafiy (Radhiya Allaahu ´anh):
“Ya kwamba siku moja alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamkuta amerukuu ambapo na yeye akarukuu nje ya safu. Kisha akajiunga ndani ya safu. Wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipotoa salamu akamwambia:
“Allaah akuzidishie pupa na usirudie.”
Hakumwamrisha kulipa Rak´ah nyingine. Alichomkataza ni kujiunga na swalah nje ya safu. Kwa hivyo ni lazima kwa ambaye amekuja kuchelewa asifanye haraka ya Rukuu´ mpaka kwanza afike katika safu.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 53-54
Imechapishwa: 01/09/2022
https://firqatunnajia.com/46-ili-mswaliji-ahesabike-amewahi-rakah-ni-lazima-awahi-kuleta-tasbiyh/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)