Swali 43: Je, ni sahihi kwamba mfungaji hahitajii kuzungusha maji mdomoni wakati wa kutawadha mchana wa Ramadhaan?
Jibu: Hilo si sahihi. Kuzungusha maji mdomoni wakati wa kutawadha ni faradhi miongoni mwa faradhi za wudhuu´. Ni mamoja mchana wa Ramadhaan au wakati mwingine kwa mfungaji na asiyekuwa mfungaji. Hilo ni kutokana na ueneaji wa maneno Yake (Ta´ala):
فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ
“… basi osheni nyuso zenu… “[1]
Lakini hatakiwi kufanya kishindo katika kuzungusha maji mdomoni au kupalizia ilihali amefunga. Hayo ni kutokana na Hadiyth ya Laqiytw bin Swabirah ambaye ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia:
“Eneza vizuri wudhuu´, asua kati ya vidole na fanya kishindo katika kupalizia isipokuwa kama utakuwa umefunga.”
[1] 05:06
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: 48 mas-alatu fiy Swiyaam, uk. 38
- Imechapishwa: 30/04/2021
Swali 43: Je, ni sahihi kwamba mfungaji hahitajii kuzungusha maji mdomoni wakati wa kutawadha mchana wa Ramadhaan?
Jibu: Hilo si sahihi. Kuzungusha maji mdomoni wakati wa kutawadha ni faradhi miongoni mwa faradhi za wudhuu´. Ni mamoja mchana wa Ramadhaan au wakati mwingine kwa mfungaji na asiyekuwa mfungaji. Hilo ni kutokana na ueneaji wa maneno Yake (Ta´ala):
فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ
“… basi osheni nyuso zenu… “[1]
Lakini hatakiwi kufanya kishindo katika kuzungusha maji mdomoni au kupalizia ilihali amefunga. Hayo ni kutokana na Hadiyth ya Laqiytw bin Swabirah ambaye ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia:
“Eneza vizuri wudhuu´, asua kati ya vidole na fanya kishindo katika kupalizia isipokuwa kama utakuwa umefunga.”
[1] 05:06
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: 48 mas-alatu fiy Swiyaam, uk. 38
Imechapishwa: 30/04/2021
https://firqatunnajia.com/43-mfungaji-hahitajii-kusukutua-mdomo-wakati-wa-kutawadha-mchana-wa-ramadhaan/