Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Dalili ni Kauli Yake (Ta´ala):
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“Mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote.”[1]
MAELEZO
Dalili ni maneno Yake (Ta´ala):
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“Mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote.”
Tumesema kuwa dalili juu ya kwamba kubwa aliloamrisha Allaah ni Tawhiyd ni maneno Yake (Ta´ala):
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“Mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote.”
Kisha akataja haki zilizobaki. Kitendo cha Yeye kuanza kutaja Tawhiyd na kukataza shirki ni dalili inayoonyesha kuwa Tawhiyd ndio kubwa aliloamrisha Allaah. Amesema:
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ
“Mwabuduni Allaah… “
akayafuatiza kwa maneno Yake:
وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“… na wala msimshirikishe na chochote.”
Haya ni makatazo. Akaanza kwa kuamrisha Tawhiyd na kukataza shirki. Kwa hiyo ikajulisha kuwa kubwa aliloamrisha Allaah ni Tawhiyd na kubwa alilokataza ni shirki. Kwa sababu Allaah ameanza kwa hayo. Haanzi (Subhaanah) isipokuwa kwa kilicho muhimu zaidi kisha yanayofuatia baada ya hapo. Hii ndio namna Aayah ilivyofahamisha.
[1] 04:36
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 90-91
- Imechapishwa: 14/12/2020
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Dalili ni Kauli Yake (Ta´ala):
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“Mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote.”[1]
MAELEZO
Dalili ni maneno Yake (Ta´ala):
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“Mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote.”
Tumesema kuwa dalili juu ya kwamba kubwa aliloamrisha Allaah ni Tawhiyd ni maneno Yake (Ta´ala):
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“Mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote.”
Kisha akataja haki zilizobaki. Kitendo cha Yeye kuanza kutaja Tawhiyd na kukataza shirki ni dalili inayoonyesha kuwa Tawhiyd ndio kubwa aliloamrisha Allaah. Amesema:
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ
“Mwabuduni Allaah… “
akayafuatiza kwa maneno Yake:
وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“… na wala msimshirikishe na chochote.”
Haya ni makatazo. Akaanza kwa kuamrisha Tawhiyd na kukataza shirki. Kwa hiyo ikajulisha kuwa kubwa aliloamrisha Allaah ni Tawhiyd na kubwa alilokataza ni shirki. Kwa sababu Allaah ameanza kwa hayo. Haanzi (Subhaanah) isipokuwa kwa kilicho muhimu zaidi kisha yanayofuatia baada ya hapo. Hii ndio namna Aayah ilivyofahamisha.
[1] 04:36
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 90-91
Imechapishwa: 14/12/2020
https://firqatunnajia.com/41-dalili-kwamba-tawhiyd-ndio-kubwa-aliloamrisha-allaah-na-shirki-ndio-kubwa-alilokataza/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)