Mashairi haya, yanayoashiria msiba ulio wazi na mkubwa, nao ni kifo cha bwana wetu, Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), yamenikumbusha ubeti niliyosoma hapo kitambo. Nayafanya ndio yenye kumalizia kitabu hiki. Nayo ni kama ifuatavyo:
Maisha haya si jengine isipokuwa ni ndoto
kila mmoja atalijua wakati atakapoiaga dunia
Anasema ´laiti kama` na nini itasaidia
kwa sababu mauti yamekwishampiga kwa mishale yake
Anatamani lau angelibaki japo kitambo kidogo
ili aweze kutubia juu ya utendaji madhambi
Ni vipi atatubia ilihali nafsi yake
Imeshakusanywa kwenye kifua chake, tayari kwa ajili ya kuondoka?
Enyi mliolala, amkeni! Mara nyingi yanaghurisha
maisha marefu ya duniani yanatangatanga
Huku wakiwa katika kughafilika
wanapigwa na kitu kinachowapooza na kuwaghafilisha
Wanawekwa ndani ya mashimo ambayo nyama zake hunyauka
na hakuna kinachobakia isipokuwa mifupa
Bali ni kwamba hata mifupa hupotea
ambayo nyuso zake zilikuwa ziking´aa gizani
Ni uzuri uliyoje ambao tulikuwa nao sote
baada ya kutuondoka, kunajitokeza upendo
Kila wanapotiwa mdomoni, shauku inaongezeka na shauku ikazidi
Kifo hiki ni cha Allaah na hakikusalimisha
si anayemcha kwa ajili ya uchaji wake wala mtenda dhambi
Endapo kingemsalimisha kiumbe yeyote
basi kingemsalimisha Mtume wa Allaah anayeheshimika
Lakini hata yeye amekunywa kwenye kikombe chake
licha ya kuwa yeye ni kipenzi cha Allaah, mbora wa viumbe
Matokeo yake ardhi ikajikusanya na kila aliye juu yake
na mawingu yakaanza kunyesha
Kila jicho likatiririka machozi na
machozi mepesi juu yake yakawa ni machozi ya furaha
Msikiti ukalia kutokana na kumpoteza
na vivyo hivyo nyumba ikalia kisha nguzo
Bali kila ardhi iliyoguswa na kuondoka kwake
baada ya nuru ikazama kwenye viza
Hakuna viumbe kama Maswahabah zake
wakati walipomuaga chini ya salamu hiyo
Wakageuka na kumuondokea,
wakiwa na huzuni na wasiweze kuongea
Kifo cha mteule ni msiba mkubwa –
wa Allaah usiofanana na mifupa
Kifo chake ni somo kubwa ambalo –
linawepesisha misiba ya wema na watu watukufu
Hata hivyo yuko hai na katika bustani kubwa la Njia
na katika cheo cha juu
Allaah amsifu kwa fadhilah Zake na amsalimishe milele
kisha jamaa zake, Maswahabah zake na wale Taabi´uun wema
Mpaka hapa kimemalizika kitabu ”Bard-ul-Akbaad ´an Faqd-il-Awlaad”. Himdi zote njema ni stahiki ya Allaah, Mola wa walimwengu. Swalah na amani zimwendee bwana wetu Muhamamd, kizazi chake na Maswahabah zake.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin ´Abdillaah bin Naaswir-id-Diyn ad-Dimashqiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bard-ul-Akbaad ´inda Faqd-il-Awlaad, uk. 128-130
- Imechapishwa: 29/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)