Swali 36: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni lini alifika Qubaa´?
Jibu: Jumatatu tarehe kumi na nane Rabiy´ al-Awwal. Hapo ndipo alipojenga msikiti wake uliokuwa umejengwa juu ya uchaji kuanzia siku ya kwanza ulipojengwa. Kwa mujibu wa maoni sahihi ndipo msikiti uliokusudiwa na Aayah (09:18). Ingawa msikiti wake aliyojenga Madiynah una haki zaidi ya kusifiwa namna hiyo.
- Muhusika: ´Allaamah Haafidhw bin Ahmad al-Hakamiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Amaaliy fiys-Siyrah an-Nabawiyyah, uk. 105
- Imechapishwa: 02/10/2023