Himdi zote njema anastahiki Allaah. Swalah na amani zimwendee Mtume wa Allaah, kizazi chake na Maswahabah zake wote.
Ama baada ya hayo;
1 – Damu yenye kutoka puani, yenye kutoka kwenye majeraha na damu ya maupele au majipu. Hizi haziathiri funga. Bali swawm ni sahihi.
2 – Damu ya ugonjwa inayomtoka mwanamke pia haiathiri funga. Bali swawm yake ni sahihi pamoja na kuendelea kwake kutoka kama ambavo haimzuii kuswali, kutufu Ka´bah na kujamiiana na mumewe. Kwa sababu damu hii haina kidhibiti. Ni damu yenye kuendelea kama kutokwa na damu puani na kwenye majeraha. Wala hakuna dalili inayofahamisha kumzuia kutokamana na ´ibaadah hizi kama ambavo dalili za wazi zimefahamisha kumzuia kutokamana na ´ibaadah hizi kwa sababu ya kuwa na hedhi na damu ya uzazi.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Duruus fiy Ramadhwaan, uk. 53
- Imechapishwa: 25/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)