Miongoni mwa adabu za swawm ni kufungua kwa tende tosa. Asipopata basi kwa tende za kawaida. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifungua kwa tende tosa kabla ya kuswali, asipopata basi kwa tende za kawaida na asipopata tende basi hunywa funda chache za maji[1].

Haitakikani kuzidisha sana aina za vyakula na vinywaji vinavyoandaliwa wakati wa kufungua, kwa sababu jambo hilo linakwenda kinyume na Sunnah na humshughulisha mtu na swalah ya mkusanyiko.

[1] Abu Daawuud (3256), at-Tirmidhiy (543), Ahmad (03/164), al-Haakim (01/432) ambaye amesema:

”Swahiyh juu ya masharti ya Muslim.”

adh-Dhahabiy ameinyamazia.

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tawjiyhaat wa Tanbiyhaat lil-Fataati al-Muslimah, uk. 33
  • Imechapishwa: 28/02/2026