31. Anayopasa mfungaji kujiepusha nayo: Mfungaji asipalizie wakati wa kutawadha

2 – Mfungaji hatakiwi kupandisha maji puani sana kwa kuchelea asije kunywa maji kwa kuingia kooni mwake. Hayo ni kutokana na yale waliyopokea waandishi wa “as-Sunan” na yakasahihishwa na Ibn Khuzaymah kupitia kwa Luqaytw aliyesimulia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia:

“Fanya kishindo katika kupalizia isipokuwa kama utakuwa umefunga.”[1]

[1] Abu Daawuud (142) na at-Tirmidhiy (788) na wengineo. at-Tirmidhiy amesema:

“Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Duruus fiy Ramadhwaan, uk. 49
  • Imechapishwa: 24/04/2023