140 –Muusa bin Ismaa´iyl amesema: Hammaad ametuhadithia, kutoka kwa ´Aliy bin Zayd, kutoka kwa Yuusuf bin Mihraan, kutoka kwa Ibn ´Abbaas ambaye amesema kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):
وَيَوْمَ تَشَقَّقُ السَّمَاءُ بِالْغَمَامِ وَنُزِّلَ الْمَلَائِكَةُ تَنزِيلًا
”Na Siku itakayofunguka mbingu kwa mawingu na Malaika watateremshwa mteremsho mkubwa wa mfuatano.”[1]
“Watashuka wakazi wa mbingu ya chini na watakuwa wengi zaidi kuliko wakazi wa ardhini katika majini na watu. Watasema wakazi wa ardhini: “Mola wetu yuko kati yenu?” Watasema: “Hapana, lakini Atakuja.” Kisha itapasuka mbingu ya pili… Kisha ipasuke mbingu ya saba. Watasema: “Mola wetu yuko kati yenu?” Watasema: “Hapana, lakini Atakuja.” Halafu baadaye Aje Allaah (´Azza wa Jall) na Malaika waliokurubishwa ambao ni wengi zaidi kuliko wakazi wa mbinguni na wakazi wa ardhini.”
Wameipokea kikosi kutoka kwa Hammaad.
141 – Muhammad bin Sa´d al-´Awfiy amesema: Baba yangu amenihadithia: Ami yangu al-Husayn bin al-Hasan bin ´Atwiyyah al-´Awfiy ametuhadithia: Baba yangu amenihadithia, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Ibn ´Abbaas ambaye amesema kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):
السَّمَاءُ مُنفَطِرٌ بِهِ ۚ كَانَ وَعْدُهُ مَفْعُولًا
”Mbingu zitapasuka hapo, ahadi Yake itatimizwa.”[2]
”Mbingu zitapasuka pindi ataposhuka Mwingi wa huruma (´Azza wa Jall.”[3]
142 – Ahmad bin Hanbal amesema katika kitabu chake “az-Zuhd”: Wakiy´ ametuhadithia: ´Aliy bin ´Aliy ametuhadithia: Nimemsikia al-Hasan akisema:
”Nimepata khabari kwamba waislamu mafukara wataingia Peponi miaka 400 kabla ya wale matajiri. Wengine watakuwa wamekaa kwa magoti yao ambapo wajiliwe na Mola (´Azza wa Jall) na aseme: ”Nyinyi mlikuwa mahakimu na watawala wa watu. Haja na matakwa Yangu yalikuwa kwenu nyinyi… Naapa kwa Allaah! Hesabu ni kali isipokuwa ile itakayofanywa wepesi na Allaah.”
143 – ´Uthmaan bin Sa´iyd ad-Daarimiy amesema:
”Maneno yake Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu ushukaji wa Allaah sio ya kushangaza kama maneno Yake (Ta´ala):
هَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا أَن يَأْتِيَهُمُ اللَّـهُ فِي ظُلَلٍ مِّنَ الْغَمَامِ وَالْمَلَائِكَةُ
”Je, wanangojea nini isipokuwa Allaah awajie katika vivuli vya mawingu pamoja na Malaika?”
na:
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا
“… na atakapokuja Mola wako na Malaika safu kwa safu.”[4]
Mwenye kuweza hilo la kwanza analiweza pia hili la pili.”[5]
144 – Harb al-Karmaaniy amesema:
”Ishaaq bin Raahuuyah amenisomea: ”Allaah (Ta´ala) amejisifu Mwenyewe ndani ya Kitabu Chake kwa sifa ambazo viumbe hawana haja ya kumsifu zaidi ya hivyo. Miongoni mwa sifa hizo ni maneno Yake:
هَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا أَن يَأْتِيَهُمُ اللَّـهُ فِي ظُلَلٍ مِّنَ الْغَمَامِ وَالْمَلَائِكَةُ
”Je, wanangojea nini isipokuwa Allaah awajie katika vivuli vya mawingu pamoja na Malaika?”
na:
وَتَرَى الْمَلَائِكَةَ حَافِّينَ مِنْ حَوْلِ الْعَرْشِ
”Utawaona Malaika wakizunguka pembezoni mwa ‘Arshi.”[6]
145 – Abu ´Umar bin ´Abdil-Wahhaab amesema: ´Abdullaah bin Ahmad bin Hanbal ametuhadithia: Ismaa´iyl bin Ahmad ametuhadithia: Nilimsomea Muhammad bin al-Qaasim: Nimemsikia Muhammad bin Aslam at-Twusiy akisema:
”Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
هَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا أَن يَأْتِيَهُمُ اللَّـهُ فِي ظُلَلٍ مِّنَ الْغَمَامِ وَالْمَلَائِكَةُ
”Je, wanangojea nini isipokuwa Allaah awajie katika vivuli vya mawingu pamoja na Malaika?”
na:
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا
“… na takapokuja Mola wako na Malaika safu kwa safu.”[7]
Yule anayekadhibisha ushukaji basi amemkadhibisha Allaah (Ta´ala) na Mtume wa Allaah (Swalla Alalahu ´alayhi wa sallam).”
[1] 25:25
[2] 73:18
[3] Jaamiy´-ul-Bayaan (29/89).
[4] 89:22
[5] ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah, uk. 47
[6] 39:75
[7] 89:22
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 145-150
- Imechapishwa: 11/06/2024
140 –Muusa bin Ismaa´iyl amesema: Hammaad ametuhadithia, kutoka kwa ´Aliy bin Zayd, kutoka kwa Yuusuf bin Mihraan, kutoka kwa Ibn ´Abbaas ambaye amesema kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):
وَيَوْمَ تَشَقَّقُ السَّمَاءُ بِالْغَمَامِ وَنُزِّلَ الْمَلَائِكَةُ تَنزِيلًا
”Na Siku itakayofunguka mbingu kwa mawingu na Malaika watateremshwa mteremsho mkubwa wa mfuatano.”[1]
“Watashuka wakazi wa mbingu ya chini na watakuwa wengi zaidi kuliko wakazi wa ardhini katika majini na watu. Watasema wakazi wa ardhini: “Mola wetu yuko kati yenu?” Watasema: “Hapana, lakini Atakuja.” Kisha itapasuka mbingu ya pili… Kisha ipasuke mbingu ya saba. Watasema: “Mola wetu yuko kati yenu?” Watasema: “Hapana, lakini Atakuja.” Halafu baadaye Aje Allaah (´Azza wa Jall) na Malaika waliokurubishwa ambao ni wengi zaidi kuliko wakazi wa mbinguni na wakazi wa ardhini.”
Wameipokea kikosi kutoka kwa Hammaad.
141 – Muhammad bin Sa´d al-´Awfiy amesema: Baba yangu amenihadithia: Ami yangu al-Husayn bin al-Hasan bin ´Atwiyyah al-´Awfiy ametuhadithia: Baba yangu amenihadithia, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Ibn ´Abbaas ambaye amesema kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):
السَّمَاءُ مُنفَطِرٌ بِهِ ۚ كَانَ وَعْدُهُ مَفْعُولًا
”Mbingu zitapasuka hapo, ahadi Yake itatimizwa.”[2]
”Mbingu zitapasuka pindi ataposhuka Mwingi wa huruma (´Azza wa Jall.”[3]
142 – Ahmad bin Hanbal amesema katika kitabu chake “az-Zuhd”: Wakiy´ ametuhadithia: ´Aliy bin ´Aliy ametuhadithia: Nimemsikia al-Hasan akisema:
”Nimepata khabari kwamba waislamu mafukara wataingia Peponi miaka 400 kabla ya wale matajiri. Wengine watakuwa wamekaa kwa magoti yao ambapo wajiliwe na Mola (´Azza wa Jall) na aseme: ”Nyinyi mlikuwa mahakimu na watawala wa watu. Haja na matakwa Yangu yalikuwa kwenu nyinyi… Naapa kwa Allaah! Hesabu ni kali isipokuwa ile itakayofanywa wepesi na Allaah.”
143 – ´Uthmaan bin Sa´iyd ad-Daarimiy amesema:
”Maneno yake Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu ushukaji wa Allaah sio ya kushangaza kama maneno Yake (Ta´ala):
هَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا أَن يَأْتِيَهُمُ اللَّـهُ فِي ظُلَلٍ مِّنَ الْغَمَامِ وَالْمَلَائِكَةُ
”Je, wanangojea nini isipokuwa Allaah awajie katika vivuli vya mawingu pamoja na Malaika?”
na:
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا
“… na atakapokuja Mola wako na Malaika safu kwa safu.”[4]
Mwenye kuweza hilo la kwanza analiweza pia hili la pili.”[5]
144 – Harb al-Karmaaniy amesema:
”Ishaaq bin Raahuuyah amenisomea: ”Allaah (Ta´ala) amejisifu Mwenyewe ndani ya Kitabu Chake kwa sifa ambazo viumbe hawana haja ya kumsifu zaidi ya hivyo. Miongoni mwa sifa hizo ni maneno Yake:
هَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا أَن يَأْتِيَهُمُ اللَّـهُ فِي ظُلَلٍ مِّنَ الْغَمَامِ وَالْمَلَائِكَةُ
”Je, wanangojea nini isipokuwa Allaah awajie katika vivuli vya mawingu pamoja na Malaika?”
na:
وَتَرَى الْمَلَائِكَةَ حَافِّينَ مِنْ حَوْلِ الْعَرْشِ
”Utawaona Malaika wakizunguka pembezoni mwa ‘Arshi.”[6]
145 – Abu ´Umar bin ´Abdil-Wahhaab amesema: ´Abdullaah bin Ahmad bin Hanbal ametuhadithia: Ismaa´iyl bin Ahmad ametuhadithia: Nilimsomea Muhammad bin al-Qaasim: Nimemsikia Muhammad bin Aslam at-Twusiy akisema:
”Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
هَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا أَن يَأْتِيَهُمُ اللَّـهُ فِي ظُلَلٍ مِّنَ الْغَمَامِ وَالْمَلَائِكَةُ
”Je, wanangojea nini isipokuwa Allaah awajie katika vivuli vya mawingu pamoja na Malaika?”
na:
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا
“… na takapokuja Mola wako na Malaika safu kwa safu.”[7]
Yule anayekadhibisha ushukaji basi amemkadhibisha Allaah (Ta´ala) na Mtume wa Allaah (Swalla Alalahu ´alayhi wa sallam).”
[1] 25:25
[2] 73:18
[3] Jaamiy´-ul-Bayaan (29/89).
[4] 89:22
[5] ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah, uk. 47
[6] 39:75
[7] 89:22
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 145-150
Imechapishwa: 11/06/2024
https://firqatunnajia.com/31-ambaye-anaweza-kushuka-anaweza-pia-kuja/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)