Swali 30: Ni yepi maoni yenu mtu kujikohozakohoza, kupuliza na kulia ndani ya swalah? Je, mambo hayo yanabatilisha swalah?
Jibu: Kujikohozakohoza, kupuliza na kulia yote hayo hayaharibu swalah. Hapana vibaya kwayo haja ikipelekea kufanya hivo. Inachukiza kuyafanya ikiwa ni pasi na haja. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alijikohozakohoza kumfanyia ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) wakati alipombishia hodi na yeye alikuwa anaswali.
Kuhusu kulia ni jambo limesuniwa katika swalah na kwenginepo kukitokana na unyenyekevu na kumwelekea Allaah pasi na kujikakama. Imesihi kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa analia ndani ya swalah. Hayo vilevile yamesihi kutoka kwa Abu Bakr as-Swiddiyq, ´Umar al-Faaruuq (Radhiya Allaahu ´anhumaa) na jopo la wengine katika Maswaahabah na waliowafuata kwa wema.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 32-33
- Imechapishwa: 22/08/2022
Swali 30: Ni yepi maoni yenu mtu kujikohozakohoza, kupuliza na kulia ndani ya swalah? Je, mambo hayo yanabatilisha swalah?
Jibu: Kujikohozakohoza, kupuliza na kulia yote hayo hayaharibu swalah. Hapana vibaya kwayo haja ikipelekea kufanya hivo. Inachukiza kuyafanya ikiwa ni pasi na haja. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alijikohozakohoza kumfanyia ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) wakati alipombishia hodi na yeye alikuwa anaswali.
Kuhusu kulia ni jambo limesuniwa katika swalah na kwenginepo kukitokana na unyenyekevu na kumwelekea Allaah pasi na kujikakama. Imesihi kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa analia ndani ya swalah. Hayo vilevile yamesihi kutoka kwa Abu Bakr as-Swiddiyq, ´Umar al-Faaruuq (Radhiya Allaahu ´anhumaa) na jopo la wengine katika Maswaahabah na waliowafuata kwa wema.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 32-33
Imechapishwa: 22/08/2022
https://firqatunnajia.com/30-swalah-ya-anayejikohozakohoza-kupuliza-na-kulia/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)