Imaam Ibn Qudaamah (Rahimahu Allaah) amesema:
رَّضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ
”Allaah amewawia radhi nao wamemridhia.”[1]
MAELEZO
5 – Kuridhia. Kuridhia ni miongoni mwa sifa za Allaah zilizothibiti kwa Qur-aan, Sunnah na maafikiano ya Salaf. Allaah (Ta´ala) amesema:
رَّضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ
”Allaah amewawia radhi nao wamemridhia.”
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah anaridhia kwa mja kuwa anapokula mlo basi akamuhimidi kwacho au akanywa kinywaji basi akamuhimidi kwacho.”[2]
Ameipokea Muslim.
Salaf wameafikiana juu ya kuthibitisha Allaah (Ta´ala) kuridhia. Kwa hiyo ni lazima kumthibitishia nayo pasi na kupotosha, kukanusha, kuifanyia namna wala kuipigia mfano. Ni kuridhia kikweli ambako kunalingana na Allaah (Ta´ala).
Ahl-ut-Ta´twiyl wamefasiri kuwa ni thawabu. Tunawaraddi kwa yale yaliyokwishatangulia katika kanuni ya nne.
[1] 5:119
[2] Muslim (2734).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 53
- Imechapishwa: 18/10/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)