6- Sahl bin al-Handhwaliyyah (Radhiya Allaahu ´anhu) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kuomba na yeye yuko na cha kumtosheleza anajikusanyia Moto.” Kukasemwa: “Ee Mtume wa Allaah! Ni kipi cha kumtosheleza?” Akasema: “Chakula cha mchana na cha jioni.”[1]
7- Ibn Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anhu) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule mwenye kuwaomba watu ilihali ana cha kumtosheleza atakuja siku ya Qiyaamah na uso wenye kuchubuka.” Kukasemwa: “Ee Mtume wa Allaah! Ni kipi chenye kutosheleza?” Akasema: “Sarafu khamsini ya fedha [dirhamu] au kiasi chake katika sarafu ya dhahabu [dinari].”[2]
Hadiyth nzuri zaidi katika mlango huu, kama alivosema ´Abdil-Barr, ni Hadiyth ya Sahl bin al-Handhwaliyyah.
8- Abu Bakr bin al-Athram ameeleza kuwa Ahmad bin Hanbal aliulizwa kuhusu kuomba na ni lini inajuzu. Akasema:
“Pale asipokuwa na chakula cha mchana wala cha jioni, kama ilivo katika Hadiyth ya Sahl bin al-Handhwaliyyah.” Akaulizwa ikiwa mtu amelazimika kuomba. Akajibu: “Inajuzu ikiwa amelazimika.” Akaulizwa ikiwa mtu ataacha kuomba katika hali hiyo. Akajibu: “Ni bora. Allaah Atamruzuku.” Kisha akasema: “Sidhani kama kuna mwenye kufa kwa sababu ya njaa.”
9- al-Athram amesema:
“Nilimsikia Ahmad akiulizwa juu ya mtu asiyepata chakula; ale nyamafu au aombe?” Akasema: “Je, ale nyamafu na wakati anaweza kuomba? Ni fedheha.”
[1] Ahmad (4/180), Abu Daawuud (1629) na Ibn Hibbaan (844).
[2] Ahmad (1/441), Abu Daawuud (1626), at-Tirmidhiy (645), an-Nasaa´iy (5/97) na Ibn Maajah (1840).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad al-Qurtwubiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Hirsw biz-Zuhd wal-Qanaa´ah, uk. 16-18
- Imechapishwa: 18/03/2017
6- Sahl bin al-Handhwaliyyah (Radhiya Allaahu ´anhu) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kuomba na yeye yuko na cha kumtosheleza anajikusanyia Moto.” Kukasemwa: “Ee Mtume wa Allaah! Ni kipi cha kumtosheleza?” Akasema: “Chakula cha mchana na cha jioni.”[1]
7- Ibn Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anhu) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule mwenye kuwaomba watu ilihali ana cha kumtosheleza atakuja siku ya Qiyaamah na uso wenye kuchubuka.” Kukasemwa: “Ee Mtume wa Allaah! Ni kipi chenye kutosheleza?” Akasema: “Sarafu khamsini ya fedha [dirhamu] au kiasi chake katika sarafu ya dhahabu [dinari].”[2]
Hadiyth nzuri zaidi katika mlango huu, kama alivosema ´Abdil-Barr, ni Hadiyth ya Sahl bin al-Handhwaliyyah.
8- Abu Bakr bin al-Athram ameeleza kuwa Ahmad bin Hanbal aliulizwa kuhusu kuomba na ni lini inajuzu. Akasema:
“Pale asipokuwa na chakula cha mchana wala cha jioni, kama ilivo katika Hadiyth ya Sahl bin al-Handhwaliyyah.” Akaulizwa ikiwa mtu amelazimika kuomba. Akajibu: “Inajuzu ikiwa amelazimika.” Akaulizwa ikiwa mtu ataacha kuomba katika hali hiyo. Akajibu: “Ni bora. Allaah Atamruzuku.” Kisha akasema: “Sidhani kama kuna mwenye kufa kwa sababu ya njaa.”
9- al-Athram amesema:
“Nilimsikia Ahmad akiulizwa juu ya mtu asiyepata chakula; ale nyamafu au aombe?” Akasema: “Je, ale nyamafu na wakati anaweza kuomba? Ni fedheha.”
[1] Ahmad (4/180), Abu Daawuud (1629) na Ibn Hibbaan (844).
[2] Ahmad (1/441), Abu Daawuud (1626), at-Tirmidhiy (645), an-Nasaa´iy (5/97) na Ibn Maajah (1840).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad al-Qurtwubiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Hirsw biz-Zuhd wal-Qanaa´ah, uk. 16-18
Imechapishwa: 18/03/2017
https://firqatunnajia.com/3-mpaka-wa-uombaji/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)