Swali 29: Ni lini majini walisikia Qur-aan? Hayo yalitokea maeneo gani?
Jibu: Hayo yalitokea katika kilimo cha mitende kati ya Makkah na at-Twaaif wakati alipokuwa njiani akirejea kutoka Thaqiyf. Miongoni mwa waliyosikia ni Suurah ”ar-Rahmaan”:
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
”Basi ni zipi katika neema za Mola wenu mnazikadhibisha?”[1]
wakasema: ”Hatukadhibishi chochote katika neema Zako, ee Mola wetu. Ni Zako himdi zote njema.”[2]
Allaah akateremsha juu ya hilo:
وَإِذْ صَرَفْنَا إِلَيْكَ نَفَرًا مِّنَ الْجِنِّ يَسْتَمِعُونَ الْقُرْآنَ فَلَمَّا حَضَرُوهُ قَالُوا أَنصِتُوا ۖ فَلَمَّا قُضِيَ وَلَّوْا إِلَىٰ قَوْمِهِم مُّنذِرِينَ
”Wakati Tulipowaelekeza kwako kundi miongoni mwa majini wakisikiliza Qur-aan, walipoihudhuria walisema: “Nyamazeni [msikilize]!” Ilipokwisha [kusomwa], waligeuka kurudi kwa watu wao wakiwaonya.”[3]
قُلْ أُوحِيَ إِلَيَّ أَنَّهُ اسْتَمَعَ نَفَرٌ مِّنَ الْجِنِّ فَقَالُوا إِنَّا سَمِعْنَا قُرْآنًا عَجَبًا
“Sema: “Nimefunuliwa Wahy ya kwamba kundi miongoni mwa majini lilisikiliza, wakasema: “Hakika sisi tumeisikia Qur-aan ya kushangaza .”[4]
[1] 55:13
[2] at-Tirmidhiy (3291) na al-Haakim (2/473).
[3] 46:29
[4] 72:1
- Mhusika: ´Allaamah Haafidhw bin Ahmad al-Hakamiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Amaaliy fiys-Siyrah an-Nabawiyyah, uk. 101
- Imechapishwa: 25/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)