Mitihani ina faida kubwa na hekima za kiungu. Baadhi yake ziko wazi kwa kufikiria, baadhi ya neema zake zinatambulika. Nyenginezo hazionekani, lakini Allaah ameiwekea fadhilah nyingi. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
فَعَسَىٰ أَن تَكْرَهُوا شَيْئًا وَيَجْعَلَ اللَّـهُ فِيهِ خَيْرًا كَثِيرًا
“… pengine ikiwa mnachukia jambo na Allaah akalijaalia ndani yake kuwa na kheri nyingi.”[1]
Imaam Ahmad amepokea katika “az-Zuhd” kutoka katika Hadiyth za al-Hasan, ambazo kuna Swahabah anayekosekana katika cheni zake za wapokezi, ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Naapa kwa Allaah! Allaah hamuadhibu mpenzi Wake, lakini anaweza kumpa mtihani duniani.”[2]
Nasema:
Mtihani unapokuwa mzito zaidi unawepesishwa kwa kuridhika
na Allaah – mwema yuko na ridhaa
Ni neema ngapi zinazoambatana na mabalaa
watu hawazioni, lakini mitihani ni zawadi
Miongoni mwa faida za mitihani ni kutafakari ufalme wa Uola na kurejea katika kujisalimisha kwa ´ibaadah. Hakuna yeyote awezaye kuepuka amri na mipango ya Allaah. Wala hakuna yeyote awezaye kukimbia hukumu na mtihani Wake wenye kutekelezeka. Ni Wake Allaah ufalme na waja. Anafanya juu yetu kile anachokitaka na vile Anavyotaka. Hakika Kwake ndio marejeo yetu katika mambo yetu yote na Kwake ndio tutakusanyika atatukusanya kwa ajili ya kutufufua.
[1] 4:19
[2] az-Zuhd, uk. 71. Kuna Swahabah anayekosekana katika cheni ya wapokezi.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin ´Abdillaah bin Naaswir-id-Diyn ad-Dimashqiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bard-ul-Akbaad ´inda Faqd-il-Awlaad, uk. 112-113
- Imechapishwa: 23/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)