Imepokelewa kwamba ash-Shaafi´iy (Rahimahu Allaah) amesema baada ya mmoja katika wanawe kuaga dunia:
Maisha si vyengine isipokuwa namna hii, hivyo subiri –
janga linaloipata mali au kutengana na kipenzi
Mtu mwenye uzoefu wa maisha haogopi
mabadiliko yake ya nyakati zake mbili kwa ajili ya mwenye busara
Muhammad bin al-Husayn bin ´Ayyaash amesema: ´Abdullaah bin Wadhdhwaah amenihadithia:
“Alisimama ´Abdul-Malik karibu na kaburi la mwanawe akasema:
Maisha na masiku si vyengine isipokuwa kama unavoona –
janga linaloipata mali au kutengana na kipenzi
Mtu mwenye uzoefu wa maisha haogopi
mabadiliko yake ya nyakati zake mbili kwa ajili ya mwenye busara
Abu Bakr bin Abiyd-Dunyaa amesema katika “Kitaab-ul-´Azaa’”: al-Husayn bin ´Abdir-Rahmaan amenihadithia kuwa bwana mmoja katika Quraysh amesema juu ya mwanawe:
Nikikupoteza wewe, ee mwanangu kipenzi, katika maisha yangu
Sintokupoteza huko Aakhirah
Ulikuwa ni kilele changu, anayeondosha hamu yangu,
matangamano yangu na anayewepesisha moyo wangu
Abu Ya´quub al-Khuraymiy akimsifu mwanawe namna hii katika shairi:
Lau isingelikuwa kutaraji malipo juu yako –
tanzia ya aliyefikwa na msiba ni kubwa
Wewe ni ukurubisho wenye kunufaisha mbele ya Allaah
na fungu letu siku ya Qiyaamah ni kubwa –
ingelidhoofika huzuni yangu, ee mwanangu kipenzi
na wale wanawake wanaolia walikuwa wamesimama kwa miguu yao
Baadhi wamesema:
Kuna faida gani ya kuomboleza wakati mtu anapoondoka?
Je, kilichopotea kitarudi kwa kunung´unika?
Yote yanahusiana na kukubali, kujisalimisha na kusubiri
kile ambacho Mungu ameshakadiria
- Mhusika: Imaam Muhammad bin ´Abdillaah bin Naaswir-id-Diyn ad-Dimashqiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bard-ul-Akbaad ´inda Faqd-il-Awlaad, uk. 111-112
- Imechapishwa: 23/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)