27- Matajiri kuchangia gharama za walima
Imependekezwa kwa wale waliofunguliwa kuchangia katika maandalizi kutokana na na Hadiyth ya Anas juu ya kisa cha yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumuoa Swafiyyah ambap alisema:
“Mpaka tulipokuwa njiani akamwandaa, yaani Umm Sulaym, kwa ajili yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akamletea naye usiku. Kwa hivyo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaamka asubuhi akiwa na bibi harusi mpya na akasema: “Yule ambaye ana kitu basi akilete.” Katika upokezi mwingine: “Yule ambaye ana kitu cha ziada basi akilete.” Anas anaendelea kusimulia: “Kwa hivyo matandiko yakatandikwa na ikawa mtu mmoja analeta maziwa makavu, mwingine analeta tende, mwingine analeta samli safi; wakafanya al-Hays (mchanganyiko wa vitu hivyo vitatu). Wakaanza kula katika al-Hays hiyo na wanakunywa kwenye vidinbwi vya maji ya mvua. Hiyo ndio ilikuwa karamu ya ndoa ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[1]
[1] Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim, Ahmad (03/102) na (195) na upokezi mwingine ni wake, Ibn Sa´d (08/122/123), al-Bayhaqiy (07/259), siyaaq ni yake na nyongeza ni ya Muslim (04/148).
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Aadaab-uz-Zafaaf, uk. 152
- Imechapishwa: 21/03/2018
27- Matajiri kuchangia gharama za walima
Imependekezwa kwa wale waliofunguliwa kuchangia katika maandalizi kutokana na na Hadiyth ya Anas juu ya kisa cha yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumuoa Swafiyyah ambap alisema:
“Mpaka tulipokuwa njiani akamwandaa, yaani Umm Sulaym, kwa ajili yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akamletea naye usiku. Kwa hivyo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaamka asubuhi akiwa na bibi harusi mpya na akasema: “Yule ambaye ana kitu basi akilete.” Katika upokezi mwingine: “Yule ambaye ana kitu cha ziada basi akilete.” Anas anaendelea kusimulia: “Kwa hivyo matandiko yakatandikwa na ikawa mtu mmoja analeta maziwa makavu, mwingine analeta tende, mwingine analeta samli safi; wakafanya al-Hays (mchanganyiko wa vitu hivyo vitatu). Wakaanza kula katika al-Hays hiyo na wanakunywa kwenye vidinbwi vya maji ya mvua. Hiyo ndio ilikuwa karamu ya ndoa ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[1]
[1] Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim, Ahmad (03/102) na (195) na upokezi mwingine ni wake, Ibn Sa´d (08/122/123), al-Bayhaqiy (07/259), siyaaq ni yake na nyongeza ni ya Muslim (04/148).
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Aadaab-uz-Zafaaf, uk. 152
Imechapishwa: 21/03/2018
https://firqatunnajia.com/29-matajiri-kuchangia-gharama-za-walima/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)