26- Kujuzu kwa walima mbali na nyama
Inajuzu kufanya karamu ya ndoa kwa chakula chochote kitachokuwa chepesi ijapokuwa kutakosekana nyama kutokana na Hadiyth ya Anas (Radhiya Allaahu ´anh) aliyesimulia:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliikaa kati ya al-Khaybar na al-Madiynah kwa muda wa siku tatu ambazo alimwingilia Swafiyyah. Akawaalika waislamu katika karamu yake ya ndoa. Hakukuweko mikate wala nyama. Kilichokuweko ni matandiko ya ngozi yalioletwa na kutandazwa na kuwekwa juu yake tende, maziwa makavu na samli safi. Watu wakala hadi wakashiba.”[1]
[1] Ameipokea al-Bukhaariy (07/387) na siyaaq ni yake, Muslim (04/147) na upokezi mwingine pamoja na nyongeza ni yake, an-Nasaa´iy (02/93), al-Bayhaqiy (07/259), Ahmad (03/259) na (264) na ana upokezi mwingine ukiwa pamoja na nyongeza.
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Aadaab-uz-Zafaaf, uk. 151
- Imechapishwa: 21/03/2018
26- Kujuzu kwa walima mbali na nyama
Inajuzu kufanya karamu ya ndoa kwa chakula chochote kitachokuwa chepesi ijapokuwa kutakosekana nyama kutokana na Hadiyth ya Anas (Radhiya Allaahu ´anh) aliyesimulia:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliikaa kati ya al-Khaybar na al-Madiynah kwa muda wa siku tatu ambazo alimwingilia Swafiyyah. Akawaalika waislamu katika karamu yake ya ndoa. Hakukuweko mikate wala nyama. Kilichokuweko ni matandiko ya ngozi yalioletwa na kutandazwa na kuwekwa juu yake tende, maziwa makavu na samli safi. Watu wakala hadi wakashiba.”[1]
[1] Ameipokea al-Bukhaariy (07/387) na siyaaq ni yake, Muslim (04/147) na upokezi mwingine pamoja na nyongeza ni yake, an-Nasaa´iy (02/93), al-Bayhaqiy (07/259), Ahmad (03/259) na (264) na ana upokezi mwingine ukiwa pamoja na nyongeza.
Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Aadaab-uz-Zafaaf, uk. 151
Imechapishwa: 21/03/2018
https://firqatunnajia.com/28-kujuzu-kufaa-kwa-walima-chakula-kingine-mbali-na-nyama/