151 – ´Awn bin Ibraahiym amenihadithia: Ahmad bin Abiyl-Hawaariy amenihadithia: ´Abdullaah bin as-Sariy amenihadithia:
”Kuna kijana mmoja alikuwa anafanya ´ibaadah huko Baswrah na shangazi yake alikuwa akimtumia chakula. Kwa muda wa siku tatu hakumwagizia chochote, ambapo akasema: ”Ee Mola, umeniondoshea riziki yangu?” Tahamaki akarushiwa mfuko wa uji kwenye kona ya msikiti, na akaambiwa: ”Hebu hii hapa, ee mchache wa subira!” Ndipo akasema: ”Naapa kwa utukufu Wako! Kwa vile Umenikaripia, basi sintokionja.”
152 – Abu Bakr bin Ismaa´iyl at-Taymiy amenihadithia: ar-Rabiy´ bin Naafiy´ ametuhadithia: ´Atwaa’ bin Muslim ametuhadithia:
”Yalipotea matumizi ya Ibraahiym bin Ad-ham, ambapo akawa anakula changarawe kwa muda wa siku kumi na tano.”
153 – al-Qaasim bin Zakariyyaa bin Diynaar al-Qurashiy ametuhadithia: Abu Yaziyd al-Mu´laa ametuhadithia: Twu´umah bin ´Amr ametuhadithia:
”Ibraahiym bin Ad-ham alikuja akiwa na njaa, ambapo akala udongo matonge matatu.”
154 – Yahyaa bin Twalhah al-Yarbuu´iy ametuhadithia: Fudhwayl bin ´Iyaadhw ametuhadithia, kutoka kwa Maalik bin Diynaar, ambaye amesema:
”Nilisema kumwambia Muhammad bin Waasiy´: ”Pepo kwa ambaye yuko na kipato cha chini.” Ndipo Muhammad akasema: ”Pepo kwa ambaye ameamka akiwa na njaa na Allaah yuko radhi naye.”
155 – Muhammad bin al-Husayn amenihadithia: Khalaf bin Ismaa´iyl amenihadithia:
”Bwana mmoja katika watu wenye hekima kutoka India alinambia: ”Kula sana kunaudhoofisha mwili.”
156 – Muhammad amenihadithia: Ahmad bin Sahl al-Urduniy amenihadithia: Nimemsikia ´Abbaad bin ´Abbaad ar-Ramliy akisema:
”Ilikuwa inasemwa kwamba kula sana kunapoteza ufahamu na kunapelekea ususuwavu na usingizi.”
157 – Muhammad amesema: Muhammad bin Ja´far al-Madaa-iniy ametuhadithia, kutoka kwa Bakr bin Khunays, kutoka kwa Abu ´Abdillaah ash-Shaamiy, kutoka kwa Mak-huul, ambaye amesema:
”´Ibaadah bora baada ya zile za faradhi, njaa na kiu.”
Bakr bin Khunays amesema:
”Ilikuwa inasemwa kwamba njaa na kiu kunamfanya mtu kufahamu vyema zaidi mawaidha na kunaulainisha moyo upesi zaidi. Ilikuwa pia inasemwa kwamba kula sana kunazuia kheri nyingi.”
158 – Ziyaad bin Ayyuub ametuhadithia: Ahmad bin Abiyl-Hawaariy ametuhadithia: Nimemsikia Abu Sulaymaan ad-Daaraaniy akisema: Nimemsikia Abul-Ash-hab, swahiba yake al-Hasan huko ´Abbaadaan, akisema:
”Allaah (´Azza wa Jall) alimfunulia wahy Daawuud (´alayhis-SalaamI): ”Ee Daawuud! Jihadhari na waonye maswahabah wako kutokana na matamanio ya chakula. Kwani hakika mioyo iliyofungamana na matamanio ya kidunia, ni yenye kuzuiwa kutokana Nami.”
- Mhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiyd-Dunyaa
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-ul-Juu´, uk. 100-103
- Imechapishwa: 25/07/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)