72- Kusimama kwenye mlima wa ´Arafah siku ya tarehe nane kwa muda fulani kwa kuchunga mwezi mwandamo usije kuonekana kimakosa.
73- Kuwasha mishumaa mingi usiku wa kuamkia ´Arafah huko Minaa.
74- Kuomba du´aa usiku wa ´Arafah kwa maneno kumi mara elfu moja:
سبحان الذي في السماء عرشه سبحان الذي في الأرض موطئه سبحان الذي في البحر سبيله
“Ametakasika ambaye ´Arshi Yake iko mbinguni. Ametakasika ambaye athari Zake ziko ardhini. Ametakasika ambaye kwenye bahari ndio kuna njia Yake… “
75- Kusafiri katika ile siku ya nane kutoka Makkah kwenda ´Arafah safari ya mara moja.
76- Kusafiri kutokea Minaa kwenda ´Arafah usiku.
77- Kuwasha moto na mishumaa kwenye mlima wa ´Arafah usiku wa ´Arafah.
78- Kuoga kwa ajili ya siku ya ´Arafah.
79- Mtu kusema wakati anapokaribia ´Arafah na akaona mlima wa Rahmah:
سبحان الله والحمد لله ولا إله إلا الله والله أكبر
“Allaah ametakasika. Himdi zote anastahiki Allaah. Hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah. Allaah ni mkubwa.”
80- Mtu kwenda kwa kukusudia ´Arafah kabla ya kuingia wakati wa kusimama, ambao ni nusu ya mchana wa ´Arafah.
81- Mtu kusema katika ´Arafah “Hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah” mara mia moja, kusoma Suurah “al-Ikhlaasw” mara mia moja kisha kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mara mia moja na mwisho wake akazidisha:
وعلينا معه
“Na juu yetu pamoja naye.”
82- Kunyamaza siku ya ´Arafah na kuacha kusoma du´aa.
83- Kupanda juu ya mlima wa Rahmah katika ´Arafah.
84- Kuingia kuba lililo katika mlima wa Rahmah ambalo wanaita kuwa ni kuba la Aadam, kuswali ndani yake na kulizunguka kama wanavyoizunguka Nyumba.
85- Kuamini kwamba Allaah (Ta´ala) hushuka jioni ya ´Arafah katika mlima wa Awraq, anapeana mikono na waliopanda vipandwa na anakumbatiana na wenye kutembea.
86- Imamu kutoa Khutbah mbili katika ´Arafah na anazipambanua baina yazo kwa kikao kama inavyofanywa katika swalah ya ijumaa.
87- Kuswali Dhuhr na ´Aswr kabla ya Khutbah.
88- Kutoa adhaana kwa ajili ya Dhuhr na ´Aswr kabla ya Khatwiyb kumaliza Khutbah yake
89- Imamu kuwaambia wakazi wa Makkah baada ya kumaliza swalah:
“Kamilisheni swalah zenu [kwa kuswali Rak´ah nne]. Kwani sisi ni wasafiri.”
90- Kuswali swalah za sunnah baina ya Dhuhr na ´Aswr katika ´Arafah.
91- Kusoma Adhkaar au du´aa maalum katika ´Arafah. Kama mfano wa du´aa ya al-Khidhr (´alayhis-Salaam) ambayo imetajwa katika “al-Ihyaa´”. Mwanzo wake ni kama ifuatavyo:
يا من لا يشغله شأن عن شأن ولا سمع عن سمع
“Ee Ambaye hushughulishwi na kitu kwa ajili ya kitu kingine wala kusikia kwa ajili ya kusikia kingine… “
Baadhi ya du´aa hizo zinafikia kurasa tano tukilinganisha na kitabu chetu hichi.
92- Baadhi ya watu kuondoka kabla ya jua kuzama.
93- Wasiokuwa wasomi wanasema kuwa kusimama ´Arafah siku ya ijumaa ni sawa na hajj sabini na mbili.
94- Kukusanyika usiku wa kuamkia mchana wa ´Arafah misikitini, au sehemu nyingine nje ya mji, kwa ajili ya kuomba du´aa na kumtaja Allaah pamoja na kunyanyua sauti juu sana, khotuba, mashairi na wanawaiga watu wa ´Arafah.
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Manaasik-ul-Hajj wal-´Umrah, uk. 51-52
- Imechapishwa: 22/07/2018
72- Kusimama kwenye mlima wa ´Arafah siku ya tarehe nane kwa muda fulani kwa kuchunga mwezi mwandamo usije kuonekana kimakosa.
73- Kuwasha mishumaa mingi usiku wa kuamkia ´Arafah huko Minaa.
74- Kuomba du´aa usiku wa ´Arafah kwa maneno kumi mara elfu moja:
سبحان الذي في السماء عرشه سبحان الذي في الأرض موطئه سبحان الذي في البحر سبيله
“Ametakasika ambaye ´Arshi Yake iko mbinguni. Ametakasika ambaye athari Zake ziko ardhini. Ametakasika ambaye kwenye bahari ndio kuna njia Yake… ”
75- Kusafiri katika ile siku ya nane kutoka Makkah kwenda ´Arafah safari ya mara moja.
76- Kusafiri kutokea Minaa kwenda ´Arafah usiku.
77- Kuwasha moto na mishumaa kwenye mlima wa ´Arafah usiku wa ´Arafah.
78- Kuoga kwa ajili ya siku ya ´Arafah.
79- Mtu kusema wakati anapokaribia ´Arafah na akaona mlima wa Rahmah:
سبحان الله والحمد لله ولا إله إلا الله والله أكبر
“Allaah ametakasika. Himdi zote anastahiki Allaah. Hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah. Allaah ni mkubwa.”
80- Mtu kwenda kwa kukusudia ´Arafah kabla ya kuingia wakati wa kusimama, ambao ni nusu ya mchana wa ´Arafah.
81- Mtu kusema katika ´Arafah “Hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah” mara mia moja, kusoma Suurah “al-Ikhlaasw” mara mia moja kisha kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mara mia moja na mwisho wake akazidisha:
وعلينا معه
“Na juu yetu pamoja naye.”
82- Kunyamaza siku ya ´Arafah na kuacha kusoma du´aa.
83- Kupanda juu ya mlima wa Rahmah katika ´Arafah.
84- Kuingia kuba lililo katika mlima wa Rahmah ambalo wanaita kuwa ni kuba la Aadam, kuswali ndani yake na kulizunguka kama wanavyoizunguka Nyumba.
85- Kuamini kwamba Allaah (Ta´ala) hushuka jioni ya ´Arafah katika mlima wa Awraq, anapeana mikono na waliopanda vipandwa na anakumbatiana na wenye kutembea.
86- Imamu kutoa Khutbah mbili katika ´Arafah na anazipambanua baina yazo kwa kikao kama inavyofanywa katika swalah ya ijumaa.
87- Kuswali Dhuhr na ´Aswr kabla ya Khutbah.
88- Kutoa adhaana kwa ajili ya Dhuhr na ´Aswr kabla ya Khatwiyb kumaliza Khutbah yake
89- Imamu kuwaambia wakazi wa Makkah baada ya kumaliza swalah:
“Kamilisheni swalah zenu [kwa kuswali Rak´ah nne]. Kwani sisi ni wasafiri.”
90- Kuswali swalah za sunnah baina ya Dhuhr na ´Aswr katika ´Arafah.
91- Kusoma Adhkaar au du´aa maalum katika ´Arafah. Kama mfano wa du´aa ya al-Khidhr (´alayhis-Salaam) ambayo imetajwa katika “al-Ihyaa´”. Mwanzo wake ni kama ifuatavyo:
يا من لا يشغله شأن عن شأن ولا سمع عن سمع
“Ee Ambaye hushughulishwi na kitu kwa ajili ya kitu kingine wala kusikia kwa ajili ya kusikia kingine… ”
Baadhi ya du´aa hizo zinafikia kurasa tano tukilinganisha na kitabu chetu hichi.
92- Baadhi ya watu kuondoka kabla ya jua kuzama.
93- Wasiokuwa wasomi wanasema kuwa kusimama ´Arafah siku ya ijumaa ni sawa na hajj sabini na mbili.
94- Kukusanyika usiku wa kuamkia mchana wa ´Arafah misikitini, au sehemu nyingine nje ya mji, kwa ajili ya kuomba du´aa na kumtaja Allaah pamoja na kunyanyua sauti juu sana, khotuba, mashairi na wanawaiga watu wa ´Arafah.
Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Manaasik-ul-Hajj wal-´Umrah, uk. 51-52
Imechapishwa: 22/07/2018
https://firqatunnajia.com/28-bidah-arafah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)