Ahl-us-Sunnah wanashuhudia ya kuwa waumini watamuona Mola wao (Tabaarak wa Ta´ala) kwa macho yao na watamtazama, kutokana na zilivyopokelewa khabari Swahiyh kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Hakika nyinyi mtamuona Mola wenu kama mnavyouona mwezi usiku wa mwezi mng´aro.”[1]
Ufananishaji uliyotajwa hapo juu ni kuhusiana na kuona na si kile kitachoonwa. Hadiyth kuhusu Kuonekana na cheni zake za wapokezi zimekaguliwa katika kitabu ”al-Intiswaar”.
[1] al-Bukhaariy (573) na Muslim (296).
- Muhusika: Imaam Abu ´Uthmaan Ismaa´iyl bin ´Abdir-Rahmaan as-Swaabuuniy (afk. 449)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ´Aqiydat-us-Salaf wa Aswhaab-il-Hadiyth, uk. 263-26
- Imechapishwa: 18/12/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)