03 – Maisha yasimame juu ya heshima, nafasi, mahaba na mapenzi
Hali ya mke iwe kama ilivopokelewa katika Hadiyth:
”… ambao anapokasirika [yule mume] anakuja na kuweka mkono wake juu ya mkono wa mume wake na kusema: “Mimi leo sionji usingizi mpaka uridhie.“[1]
Hii ndio hali ya mke mwema. Ni mamoja yeye ndiye amedhulumu au amedhulumiwa.
Na hali ya mume iyakariri maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Muumini mwanaume asimchukie muumini mwanamke. Akichukia kutoka kwake tabia fulani basi ataridhia nyingine.”[2]
Ameipokea Ahmad na Muslim.
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Mbora wenu ni yule mbora wenu kwa famili yake na mimi ni mbora wenu kwa familia yangu.”[3]
Ibn Maajah na at-Tirmidhiy.
[1] al-Bayhaqiy katika ”Shu´ab-ul-Iymaan” (11/171) (8358).
[2] Muslim (1469), at-Tirmidhiy (3895) na Ibn Maajah (1977).
[3] at-Tirmidhiy (3895) na Ibn Maajah (1977). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Ibn Maajah” (1608).
- Muhusika: Shaykh Jamaal bin Furahyaan al-Haarithiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Twalaaq – asbaabuhu wa ´ilaajuh, uk. 41-42
- Imechapishwa: 23/04/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)