Imaam Ibn Qudaamah (Rahimahu Allaah) amesema:
بَلْ يَدَاهُ مَبْسُوطَتَانِ
”Bali mikono Yake imefumbuliwa.”[1]
MAELEZO
2 – Mikono miwili. Mikono miwili ni miongoni mwa sifa za Allaah zilizothibiti kwa Qur-aan, Sunnah na maafikiano ya Salaf. Allaah (Ta´ala) amesema:
بَلْ يَدَاهُ مَبْسُوطَتَانِ
”Bali mikono Yake imefumbuliwa.”[2]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mkono wa kuume wa Allaah umejaa. Haupungui kwa kutoa usiku na mchana.” Mpaka aliposema: “Kwa mkono Wake mwingine anakamata; anainua na anashusha.”[3]
Ameipokea Muslim na al-Bukhaariy amepokea maana yake.
Salaf wameafikiana juu ya kumthibitishia Allaah (Ta´ala) mikono miwili. Kwa hiyo ni lazima kumthibitishia nayo pasi na kupotosha, kukanusha, kuifanyia namna wala kuipigia mfano. Ni mikono miwili ya Allaah ya kikweli inayolingana Naye.
Ahl-ut-Ta´twiyl wameifasiri kuwa ni neema, uwezo na mfano wake. Tunawaraddi kwa yale yaliyokwishatangulia katika kanuni ya nne. Kuna njia nyingine ya nne; nayo ni kwamba katika mtiririko wa maneno kuna yanayozuia kabisa kufasiri namna hiyo. Amesema (Ta´ala):
قَالَ يَا إِبْلِيسُ مَا مَنَعَكَ أَن تَسْجُدَ لِمَا خَلَقْتُ بِيَدَيَّ
”Kipi kilichokuzuia usimsujudie Niliyemuumba kwa mikono Yangu?”[4]
Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kwa mkono Wake mwingine anakamata; anainua na anashusha.”
[1] 05:64
[2] 05:64
[3] Muslim (993) na al-Bukhaariy (4684).
[4] 38:75
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 49-50
- Imechapishwa: 17/10/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)