117 – Yaziyd bin Haaruun ametuhadithia: al-´Awaam bin Hawshab ametueleza, kutoka kwa Abu Swaadiq, kutoka kwa´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh), ambaye amesema:
”Hakika imani ina sehemu tatu: imani, swalah na mkusanyiko. Swalah haikubaliwi pasi na imani. Mwenye kuamini, basi huswali. Mwenye kuswali, hushikana na mkusanyiko. Yule mwenye kutengana na mkusanyiko kiasi cha shibiri, basi ameng´oa kitanzi cha Uislamu kutoka shingoni mwake.”[1]
118 – Yaziyd bin Haaruun ametuhadithia: Muhammad bin Mutwarrif ametueleza, kutoka kwa Hassaan bin ´Atwiyyah, kutoka kwa Abu Umaamah, ambaye ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Hayaa na kutokusema[2] ni tanzu mbili za imani.”[3]
[1] Cheni ya wapokezi ni yenye kukatika kati ya Abu Swaadiq na ´Aliy, kama ilivyo katika ”at-Taqriyb”.
[2] Bi maana kuchunga ulimi kutozungumza uwongo. Haihusiani na kunyamaza kwa moyo, kunyamaza kwa matendo wala kunyamaza kwa ulimi kutokana na kasoro, kama alivosema al-Munaawiy.
[3] Cheni ya wapokezi ni Swahiyh. at-Tirmidhiy ameipokea kupitia njia nyingine, kutoka kwa Yaziyd bin Haaruun, na akasema:
”Hadiyth ni nzuri na geni. Kutokusema ni uchache wa kuzungumza.”
Uzindushi imekuja katika ile ya asili baada ya Muhammad bin Mutwarrif “kutoka kwa Yaziyd”. Nikaifuta kwa sababu haipo katika ”al-Muswannaf”, at-Tirmidhiy wala kwenginepo.
- Mhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiy Shaybah al-Kuufiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-ul-Iymaan, uk. 44
- Imechapishwa: 17/07/2023
- taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)