Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akikusanya Suurah zinazofanana[1] kuanzia mwanzo wa Suurah Qaaf mpaka mwisho wa Qur-aan. Alikuwa anaweza kusoma “ar-Rahmaan” na “an-Najm” katika Rak´ah moja[2], “al-Qamar” na “al-Haaqqah” katika Rak´ah moja, “at-Twuur” na “adh-Dhaariyaat” katika Rak´ah moja, “al-Waaqi´ah” na “al-Qalam” katika Rak´ah moja, “al-Ma´aarij” na “an-Naazi´aat” katika Rak´ah moja, “al-Mutwaffifiyn” na “´Abasa” katika Rak´ah moja, “al-Mudaththir” na “al-Muzammil” katika Rak´ah moja, “al-Insaan” na “al-Qiyaamah” katika Rak´ah moja, “an-Naba´” na “al-Mursalaat” katika Rak´ah moja, “ad-Dukhaan” na “at-Takwiyr” katika Rak´ah moja[3].
Wakati mwingine alikuwa anaweza kukusanya Suurah saba ndefu kama “al-Baqarah”, “an-Nisaa´” na “Aal ´Imraan” katika Rak´ah moja katika swalah ya usiku. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swalah bora ni ile yenye kisimamo kirefu zaidi.”[4]
Baada ya kusoma:
أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ
“Je, huyo hakuwa ni muweza wa kuhuisha wafu?”[5]
husema:
سبحانك فَبَلى
“Kutakasika ni Kwako kutokamana na mapungufu; ndio.”
Na anaposoma:
سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى
“Limetakasika Jina la Mola wako Aliye juu?”[6]
husema:
سبحان ربي الأعلى
“Ametakasika kutokamana na mapungufu, Mola Aliye juu.”[7]
[1] Bi maana Suurah zinazofanana katika maana kama mawaidha, maamrisho au visa.
[2] Hili linafahahamisha kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mara nyingi hakuwa akijali kusoma Suurah kwa mpangilio uliyoko katika Qur-aan. Inaonyesha kuwa ni jambo linaloruhusiwa. Litatajwa wakati wa swalah ya usku, inagawa ni bora zaidi kufuata upangiliaji.
[3] al-Bukhaariy na Muslim.
[4] Muslim na at-Twahaawiy.
[5] 75:40
[6] 87:01
[7] Abu Daawuud na al-Bayhaqiy kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh. Hadiyth hii imeachwa na hivyo inajumuisha kisomo kisomo cha Qur-aan katika swalah na nje ya swalah, katika swalah ya Sunnah au ya faradhi. Ibn Abiy Shaybah (02/132/2) amepokea ya kwamba Abu Muusa al-Ash´ariy na al-Mughiyrah (Radhiya Allaahu ´anhumaa) walikuwa wakiisema katika swalah ya faradhi. Kadhalika wameipokea kwa kuachia kutoka kwa ´Umar na ´Aliy.
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 91-92
- Imechapishwa: 04/02/2017
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akikusanya Suurah zinazofanana[1] kuanzia mwanzo wa Suurah Qaaf mpaka mwisho wa Qur-aan. Alikuwa anaweza kusoma “ar-Rahmaan” na “an-Najm” katika Rak´ah moja[2], “al-Qamar” na “al-Haaqqah” katika Rak´ah moja, “at-Twuur” na “adh-Dhaariyaat” katika Rak´ah moja, “al-Waaqi´ah” na “al-Qalam” katika Rak´ah moja, “al-Ma´aarij” na “an-Naazi´aat” katika Rak´ah moja, “al-Mutwaffifiyn” na “´Abasa” katika Rak´ah moja, “al-Mudaththir” na “al-Muzammil” katika Rak´ah moja, “al-Insaan” na “al-Qiyaamah” katika Rak´ah moja, “an-Naba´” na “al-Mursalaat” katika Rak´ah moja, “ad-Dukhaan” na “at-Takwiyr” katika Rak´ah moja[3].
Wakati mwingine alikuwa anaweza kukusanya Suurah saba ndefu kama “al-Baqarah”, “an-Nisaa´” na “Aal ´Imraan” katika Rak´ah moja katika swalah ya usiku. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swalah bora ni ile yenye kisimamo kirefu zaidi.”[4]
Baada ya kusoma:
أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ
“Je, huyo hakuwa ni muweza wa kuhuisha wafu?”[5]
husema:
سبحانك فَبَلى
“Kutakasika ni Kwako kutokamana na mapungufu; ndio.”
Na anaposoma:
سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى
“Limetakasika Jina la Mola wako Aliye juu?”[6]
husema:
سبحان ربي الأعلى
“Ametakasika kutokamana na mapungufu, Mola Aliye juu.”[7]
[1] Bi maana Suurah zinazofanana katika maana kama mawaidha, maamrisho au visa.
[2] Hili linafahahamisha kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mara nyingi hakuwa akijali kusoma Suurah kwa mpangilio uliyoko katika Qur-aan. Inaonyesha kuwa ni jambo linaloruhusiwa. Litatajwa wakati wa swalah ya usku, inagawa ni bora zaidi kufuata upangiliaji.
[3] al-Bukhaariy na Muslim.
[4] Muslim na at-Twahaawiy.
[5] 75:40
[6] 87:01
[7] Abu Daawuud na al-Bayhaqiy kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh. Hadiyth hii imeachwa na hivyo inajumuisha kisomo kisomo cha Qur-aan katika swalah na nje ya swalah, katika swalah ya Sunnah au ya faradhi. Ibn Abiy Shaybah (02/132/2) amepokea ya kwamba Abu Muusa al-Ash´ariy na al-Mughiyrah (Radhiya Allaahu ´anhumaa) walikuwa wakiisema katika swalah ya faradhi. Kadhalika wameipokea kwa kuachia kutoka kwa ´Umar na ´Aliy.
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 91-92
Imechapishwa: 04/02/2017
https://firqatunnajia.com/25-kukusanya-kati-ya-suurah-mbili-zinazofanana-katika-rakah-moja/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)