25. Hadiyth ”Mola wetu atafunua muundi Wake… ”

Hadiyth ya kumi

يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ

“Siku utakapofunuliwa muundi.”[1]

113 – Yuusuf bin Abiy Naswr ametukhabarisha, Abul-Fadhl Ahmad bin Hibatillaah na Ismaa´iyl bin ´Abdir-Rahmaan wametuhadithia: al-Husayn bin al-Mubaarak ametuhadithia: ´Abdul-Awwal bin ´Iysaa ametuhadithia: Abul-Hasan al-Mudhwaffariy ametuhadithia: Abu Muhammad al-Hamuuyiy ametuhadithia: Abu ´Abdillaah al-Matwariy ametuhadithia: Abu ´Abdillaah al-Bukhaariy ametuhadithia: Yahyaa bin Bukayr ametuhadithia: al-Layth ametuhadithia, kutoka kwa Khaalid bin Yaziyd, kutoka kwa Sa´iyd bin Abiy Hilaal, kutoka kwa Zayd, kutoka kwa ´Atwaa’ bin Yasaar, kutoka kwa Abu Sa´iyd aliyesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuhusu Uombezi:

”Ndipo atafunua muundi Wake (´Azza wa Jall) na amsujudie kila muumini.”[2]

114 – Aadam bin Abiy Iyaas kutoka kwa Abu ´Umar as-Swan´aaniy, kutoka kwa Zayd bin Aslam amepokea mfano wake kwa tamko lisemalo:

”Mola wetu atafunua muundi Wake na hakutobaki yeyote aliyemsujudia kwa kutaka kwake mwenyewe duniani, isipokuwa ataidhinishwa kumsujudia tena.”

Ameipokea al-Bukhaariy katika ”as-Swahiyh” yake.

115 – Ibn-ul-Baylamaaniy amepokea kuwa Ibn ´Umar amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):

يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ

“Siku utakapofunuliwa muundi.”

 “Mola wetu atafunua muundi Wake ambapo tutamporomokea kumsujudia.”[3]

116 – Salamah bin Kuhayl amesimulia kuwa Abu Swaadiq, kutoka kwa Ibn Mas´uud ambaye amesema kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):

يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ

“Siku utakapofunuliwa muundi.”

”Bi maana muundi Wake (´Azza wa Jall).”

118 – al-Minhaal bin ´Amr amepokea kutoka kwa Abu ´Ubaydah bin ´Abdillaah bin Mas´uud, kutoka kwa Masruuq, kutoka kwa Ibn Mas´uud, kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amesema:

”Allaah atawakusanya wa mwanzo na wa mwisho na atashuka katika vivuli vya mawingu, kutoka katika ´Arshi kwenda katika Kursiy. Atawaendea na aseme: ”Ni kwa nini hamwondoki?” Watasema: ”Sisi tunaye Mungu ambaye bado hatujamuona.” Ndipo aseme: ”Je, mtamjua pindi mtakapomuona?” Waseme: ”Ndio. Kuna alama baina yetu sisi na Yeye; tutapoiona tutamjua.” Atasema: ”Ni ipi?” Watasema: ”Atafunua muundi Wake.” Hapo ndipo atafunua muundi Wake.”

Ameipokea al-Khallaal katika ”as-Sunnah” kupitia kwa al-Marruudhiy, kutoka kwa Ismaa´iyl bin Abiy Kariymah al-Harraaniy, kutoka kwa Muhammad bin Salamah, kutoka kwa Khaalid bin Abiy Yaziyd, kutoka kwa Zayd bin Abiy Aniysah, kutoka kwa al-Minhaal bin ´Amr.

Hadiyth ni Swahiyh.

[1] 68:42

[2] al-Bukhaariy, Ibn ´Awaanah, Muslim, Ibn Khuzaymah katika ”Kitaab-ut-Tawhiyd” na al-Haakim.

[3] ad-Daaraqutwniy katika “ar-Ru’yah”, uk. 147

  • Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 116-122
  • Imechapishwa: 09/06/2024