Swali 23: Ni kipi walichofanya washirikina wakati walipoona jambo hilo?
Jibu: Walikusanyika juu ya kuacha kuchaganyika, kuwazungumzisha na kuoa kutoka kwa Banuu Haashim na Banuu ´Abdil-Muttwalib. Washirikina wakaandika mkataba walioutundika juu ya ukuta wa Ka´bah. Kwa hivyo Banuu Haashim na Banuu ´Abdil-Muttwalib walikutana katika kifungu cha Abu Twaalib ili kujadili hali waliyomo.
- Muhusika: ´Allaamah Haafidhw bin Ahmad al-Hakamiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Amaaliy fiys-Siyrah an-Nabawiyyah, uk. 98
- Imechapishwa: 19/09/2023