Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
La pili: Hakika Allaah haridhii kushirikishwa pamoja Naye yeyote katika ´ibaadah Yake;
MAELEZO
Suala hili limefungamana na suala la kwanza. Kwa sababu suala la kwanza linabainisha ulazima wa kumwabudu Allaah na kumfuata Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hiyo ndio maana ya kushuhudia ya kwamba hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah.
Suala la pili ni kwamba ´ibaadah ikichanganyikana na shirki haikubaliwi. Ni lazima ´ibaadah iwe imefanywa kwa ajili ya kutafuta uso wa Allaah (´Azza wa Jall) pekee. Kwa hiyo yule mwenye kumwabudu Allaah na wakati huohuo akamwabudu mwengine basi ´ibaadah yake ni batili. Upatikani wake ni sawa na ukosekanaji wake. Kwa sababu ´ibaadah hainufaishi isipokuwa pamoja na Ikhlaasw na Tawhiyd. Ikichanganyikana na shirki basi inaharibika. Amesema (Ta´ala):
وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ
“Hakika umefunuliwa Wahy na kwa wale walio kabla yako kwamba: “Ukifanya shirki bila shaka yataporomoka matendo yako na hakika utakuwa miongoni mwa waliokhasirika.”[1]
وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ
“Lau wangemshirikisha bila shaka yangeporomoka yale waliyokuwa wakitenda.”[2]
´Ibaadah haiitwi ´ibaadah isipokuwa ikiambatana na Tawhiyd kama ambavo swalah haiitwi kuwa ni swalah isipokuwa ikiambatana na twahara. Shirki ikichanganyikana na ´ibaadah inaiharibu. Ni kama ambavo twahara ikichanganyikana na moja katika vichenguzi vya wudhuu´ basi inaiharibu na kuibatilisha. Kwa ajili hiyo ndio maana utaona Allaah katika Aayah nyingi anakusanya kati ya amri ya kumwabudu Yeye na makatazo ya shirki. Amesema (Ta´ala):
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“Mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe Yeye na chochote.”[3]
وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ
“Hawakuamrishwa jengine isipokuwa wamuabudu Allaah pekee hali ya kumtakasia yeye dini, wenye kupondoka kwenye haki na kuiacha batili.”[4]
وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ
“Hatukutuma kabla yako Mtume yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Mimi; hivyo basi niabuduni.”[5]
Maneno Yake (Ta´ala):
لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ
“Hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Mimi; hivyo basi niabuduni.”
kuna amri mbili:
1- Kuna makanusho ya shirki.
2- Kuna kumthibitishia ´ibaadah Allaah (Ta´ala).
Amesema (Ta´ala):
وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ
“Mola wako ameamuru kwamba: “Msiabudu yeyote isipokuwa Yeye pekee.”[6]
وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ
”Hakika Tulituma katika kila ummah Mtume kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na Twaaghuut [waungu batili].”[7]
Kumeambatanishwa kati ya kumwabudu Allaah na kuepuka Twaaghuut.
[1] 39:65
[2] 06:88
[3] 04:36
[4] 98:05
[5] 21:25
[6] 17:23
[7] 16:36
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 52-54
- Imechapishwa: 02/12/2020
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
La pili: Hakika Allaah haridhii kushirikishwa pamoja Naye yeyote katika ´ibaadah Yake;
MAELEZO
Suala hili limefungamana na suala la kwanza. Kwa sababu suala la kwanza linabainisha ulazima wa kumwabudu Allaah na kumfuata Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hiyo ndio maana ya kushuhudia ya kwamba hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah.
Suala la pili ni kwamba ´ibaadah ikichanganyikana na shirki haikubaliwi. Ni lazima ´ibaadah iwe imefanywa kwa ajili ya kutafuta uso wa Allaah (´Azza wa Jall) pekee. Kwa hiyo yule mwenye kumwabudu Allaah na wakati huohuo akamwabudu mwengine basi ´ibaadah yake ni batili. Upatikani wake ni sawa na ukosekanaji wake. Kwa sababu ´ibaadah hainufaishi isipokuwa pamoja na Ikhlaasw na Tawhiyd. Ikichanganyikana na shirki basi inaharibika. Amesema (Ta´ala):
وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ
“Hakika umefunuliwa Wahy na kwa wale walio kabla yako kwamba: “Ukifanya shirki bila shaka yataporomoka matendo yako na hakika utakuwa miongoni mwa waliokhasirika.”[1]
وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ
“Lau wangemshirikisha bila shaka yangeporomoka yale waliyokuwa wakitenda.”[2]
´Ibaadah haiitwi ´ibaadah isipokuwa ikiambatana na Tawhiyd kama ambavo swalah haiitwi kuwa ni swalah isipokuwa ikiambatana na twahara. Shirki ikichanganyikana na ´ibaadah inaiharibu. Ni kama ambavo twahara ikichanganyikana na moja katika vichenguzi vya wudhuu´ basi inaiharibu na kuibatilisha. Kwa ajili hiyo ndio maana utaona Allaah katika Aayah nyingi anakusanya kati ya amri ya kumwabudu Yeye na makatazo ya shirki. Amesema (Ta´ala):
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“Mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe Yeye na chochote.”[3]
وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ
“Hawakuamrishwa jengine isipokuwa wamuabudu Allaah pekee hali ya kumtakasia yeye dini, wenye kupondoka kwenye haki na kuiacha batili.”[4]
وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ
“Hatukutuma kabla yako Mtume yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Mimi; hivyo basi niabuduni.”[5]
Maneno Yake (Ta´ala):
لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ
“Hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Mimi; hivyo basi niabuduni.”
kuna amri mbili:
1- Kuna makanusho ya shirki.
2- Kuna kumthibitishia ´ibaadah Allaah (Ta´ala).
Amesema (Ta´ala):
وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ
“Mola wako ameamuru kwamba: “Msiabudu yeyote isipokuwa Yeye pekee.”[6]
وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ
”Hakika Tulituma katika kila ummah Mtume kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na Twaaghuut [waungu batili].”[7]
Kumeambatanishwa kati ya kumwabudu Allaah na kuepuka Twaaghuut.
[1] 39:65
[2] 06:88
[3] 04:36
[4] 98:05
[5] 21:25
[6] 17:23
[7] 16:36
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 52-54
Imechapishwa: 02/12/2020
https://firqatunnajia.com/23-allaah-haridhii-kushirikishwa-pamoja-naye-yeyote-katika-ibaadah-yake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)