3 – Miongoni mwa maneno ya wanafunzi wa wanafunzi wa Maswahabah amesema al-Awzaa´iy ´Abdur-Rahmaan bin ´Amr ambaye amekufa mwaka wa 157:
“Lazimiana na Aathaar za waliotangulia… “
Lazimiana na njia ya Maswahabah na wale waliowafata kwa wema kwa sababu wamejengeka juu ya Qur-aan na Sunnah.
“… hata kama watu watakukataa… “
Bi maana watakutenga na kujiweka mbali nawe.
“… na jihadhari na maoni ya watu… “
Tahadhari na maoni ya watu. Nayo ni yale yaliyosemwa kwa maoni tu pasi na kutegemea Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
“… hata kama watakupambia kwa maneno.”
Watakupambia na kuyafanya vizuri matamshi. Batili haigeuki kuwa haki kwa kupambwa na kufanywa nzuri.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 43-44
- Imechapishwa: 17/10/2022
3 – Miongoni mwa maneno ya wanafunzi wa wanafunzi wa Maswahabah amesema al-Awzaa´iy ´Abdur-Rahmaan bin ´Amr ambaye amekufa mwaka wa 157:
“Lazimiana na Aathaar za waliotangulia… “
Lazimiana na njia ya Maswahabah na wale waliowafata kwa wema kwa sababu wamejengeka juu ya Qur-aan na Sunnah.
“… hata kama watu watakukataa… “
Bi maana watakutenga na kujiweka mbali nawe.
“… na jihadhari na maoni ya watu… “
Tahadhari na maoni ya watu. Nayo ni yale yaliyosemwa kwa maoni tu pasi na kutegemea Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
“… hata kama watakupambia kwa maneno.”
Watakupambia na kuyafanya vizuri matamshi. Batili haigeuki kuwa haki kwa kupambwa na kufanywa nzuri.
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 43-44
Imechapishwa: 17/10/2022
https://firqatunnajia.com/23-al-awzaaiy-akihimiza-sunnah-na-akitahadharisha-bidah/