06 – Kutazama vipindi vya mwendelezo na filamu zisizokuwa na maadili

Miongoni mwa makosa yanayoenda kinyume na Shari´ah ni kutazama yale aliyoharamisha Allaah katika vipindi vya mwendelezo, filamu zisizokuwa na maadili na magazeti yanayoita katika kila uovu na kuonya kutokana na kila sifa tukufu. Hivyo basi mche Allaah, ee mjakazi wa Allaah, na tambua ya kwamba utaulizwa juu ya jambo hili. Amesema (Ta´ala):

إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْؤُولاً

“Hakika masikio na macho na moyo, vyote hivyo vitaulizwa.”[1]

[1] 17:36

  • Muhusika: Dr. ´Abdul-´Aziyz bin Daawuud al-Faaiz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tawjiyhaat wa Tanbiyhaat lil-Fataati al-Muslimah, uk. 27
  • Imechapishwa: 17/02/2026