05 – Viatu vyenye kisigino kirefu

Miongoni mwa makosa yanayoenda kinyume na Shari´ah ni kuvaa viatu vyenye kisigino kirefu, jambo ambalo halijuzu. Kufanya hivo ni katika kuonyesha mapambo, jambo ambalo Allaah amelikataza pale aliposema:

وَلَا تَبَرَّجْنَ تَبَرُّجَ الْجَاهِلِيَّةِ الْأُولَىٰ

“… na wala msijishauwe mshauwo wa wanawake majahili wa awali.”[1]

Bali wanazuoni wamesema kuwa ikiwa viatu hivyo vitakuwa na sauti basi ni haramu zaidi kuliko hata vikuku.

[1] 33:33

  • Muhusika: Dr. ´Abdul-´Aziyz bin Daawuud al-Faaiz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tawjiyhaat wa Tanbiyhaat lil-Fataati al-Muslimah, uk. 27
  • Imechapishwa: 17/02/2026