Swali 21: Naona katikati ya swalah ya ijumaa katika misikiti miwili Mitakatifu baadhi ya watu wanasimama kwa ajili ya kuswali Rak´ah mbili baada ya muadhini kumaliza kutoa adhaana ya kwanza. Nataraji kutoka kwa muheshimiwa kubainisha haki juu ya kitendo hichi. Allaah akujaze kheri na aurefushe umri wako katika kumtii[1].
Jibu: Sitambui katika dalili za Shari´ah yanayofahamisha juu ya kupendekeza kwa Rak´ah mbili hizi. Kwa sababu adhaana iliyotajwa ilianzishwa na ´Uthmaan bin ´Affaan (Radhiya Allaahu ´anh) wakati wa uongozi wake pindi watu walipokuwa wengi Madiynah. Alicholenga ni kuwazindua kwamba siku ya leo ni ya ijumaa na Maswahabah wakamfata katika jambo hilo. Miongoni mwao ni ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh). Jambo likatulia juu ya kwamba ni Sunnah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Lazimianeni na Sunnah zangu na Sunnah za makhaliyfah wangu waongofu. Ziumeni kwa magego yenu.”[2]
Baadhi ya wanazuoni wameona kuwa Rak´ah mbili hizi baada ya adhaana zimesuniwa kutokana na kuenea kwa maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kati ya kila adhaana mbili kuna swalah. Kati ya kila adhaana mbili kuna swalah.” Kisha mara ya tatu akasema: “Kwa anayetaka.”[3]
Inavyonidhihirikia ni kwamba adhaana iliyotajwa haingii katika hilo. Kwa sababu makusudio ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliposema “adhaana mbili” ni adhaana na Iqaamah tukiondosha siku ya ijumaa. Kuhusu siku ya ijumaa imewekwa katika Shari´ah kwa watu kujiandaa kusikiliza Khutbah baada ya adhaana.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (12/390-391).
[2] Abu Daawuud (4607).
[3] al-Bukhaariy (588, 591) na tamko ni lake na Muslim (1384).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam Swalaat-il-Jumu´ah wal-Jamaa´ah, uk. 61-62
- Imechapishwa: 28/11/2021
Swali 21: Naona katikati ya swalah ya ijumaa katika misikiti miwili Mitakatifu baadhi ya watu wanasimama kwa ajili ya kuswali Rak´ah mbili baada ya muadhini kumaliza kutoa adhaana ya kwanza. Nataraji kutoka kwa muheshimiwa kubainisha haki juu ya kitendo hichi. Allaah akujaze kheri na aurefushe umri wako katika kumtii[1].
Jibu: Sitambui katika dalili za Shari´ah yanayofahamisha juu ya kupendekeza kwa Rak´ah mbili hizi. Kwa sababu adhaana iliyotajwa ilianzishwa na ´Uthmaan bin ´Affaan (Radhiya Allaahu ´anh) wakati wa uongozi wake pindi watu walipokuwa wengi Madiynah. Alicholenga ni kuwazindua kwamba siku ya leo ni ya ijumaa na Maswahabah wakamfata katika jambo hilo. Miongoni mwao ni ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh). Jambo likatulia juu ya kwamba ni Sunnah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Lazimianeni na Sunnah zangu na Sunnah za makhaliyfah wangu waongofu. Ziumeni kwa magego yenu.”[2]
Baadhi ya wanazuoni wameona kuwa Rak´ah mbili hizi baada ya adhaana zimesuniwa kutokana na kuenea kwa maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kati ya kila adhaana mbili kuna swalah. Kati ya kila adhaana mbili kuna swalah.” Kisha mara ya tatu akasema: “Kwa anayetaka.”[3]
Inavyonidhihirikia ni kwamba adhaana iliyotajwa haingii katika hilo. Kwa sababu makusudio ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliposema “adhaana mbili” ni adhaana na Iqaamah tukiondosha siku ya ijumaa. Kuhusu siku ya ijumaa imewekwa katika Shari´ah kwa watu kujiandaa kusikiliza Khutbah baada ya adhaana.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (12/390-391).
[2] Abu Daawuud (4607).
[3] al-Bukhaariy (588, 591) na tamko ni lake na Muslim (1384).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahkaam Swalaat-il-Jumu´ah wal-Jamaa´ah, uk. 61-62
Imechapishwa: 28/11/2021
https://firqatunnajia.com/21-kuswali-rakah-mbili-baada-ya-adhaana-ya-kwanza-ya-ijumaa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)