18 – Abu Hurayrah amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mbali na wale Malaika wanaoandika matendo ya watu Allaah anao Malaika wanaozunguka ardhini. Wanapowapata watu wanaomdhukuru Allaah (Ta´ala) wanaita: “Njooni katika utashi wenu!” Kisha wanawazunguka. Wanapotawanyika wanapanda mbinguni ambapo Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) anasema: “Mmewaacha waja wangu wanafanya nini mlipowaacha?” Wanasema: “Tumewaacha wanakuhimidi, wanakutukuza na wanakutaja.” Ndipo aseme: “Kwani wamekwishaniona?” Wanasema: “Hapana.”Aseme: “Vipi lau wangeniona?” Waseme: “Lau wangekuona basi wangekuhimidi, kukutukuza na kukutaja kwa wingi kulikoni.” Aseme: “Kwani wanatafuta nini?” Waseme: “Wanatafuta Pepo.” Aseme: “Wamekwishaiona?” Waseme: “Hapana.” Aseme: “Vipi lau wangeiona?” Waseme: “Wangeiona basi wangelikuwa na bidii zaidi kulikoni.” Aseme: “Wanajilinda kutokamana na nini?” Waseme: “Wanajilinda kutokamana na Moto.” Aseme: “Kwani wamekwishauona?” Waseme: “Hapana.” Aseme: “Vipi wangeuona?” Waseme: “Wangeuona basi wangeukimbia na kujilinda nao zaidi kulikoni.” Ndipo aseme: “Mimi nakushuhudisheni kwamba nimewasamehe.” Waseme: “Wako ambao wameingia kimakosa. Wameingia humo kwa ajili tu ya haja.” Aseme: “Ni watu ambao matangamano yao si yenye kula khasara. Ni watu ambao matangamano yao si yenye kula khasara.”[1]
Ameipokea av al-Bukhaariy na Muslim.
[1] al-Bukhaariy (6408), Muslim (4689) na at-Tirmidhiy (3600).
- Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk 90-91
- Imechapishwa: 12/04/2024
- taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
18 – Abu Hurayrah amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mbali na wale Malaika wanaoandika matendo ya watu Allaah anao Malaika wanaozunguka ardhini. Wanapowapata watu wanaomdhukuru Allaah (Ta´ala) wanaita: “Njooni katika utashi wenu!” Kisha wanawazunguka. Wanapotawanyika wanapanda mbinguni ambapo Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) anasema: “Mmewaacha waja wangu wanafanya nini mlipowaacha?” Wanasema: “Tumewaacha wanakuhimidi, wanakutukuza na wanakutaja.” Ndipo aseme: “Kwani wamekwishaniona?” Wanasema: “Hapana.”Aseme: “Vipi lau wangeniona?” Waseme: “Lau wangekuona basi wangekuhimidi, kukutukuza na kukutaja kwa wingi kulikoni.” Aseme: “Kwani wanatafuta nini?” Waseme: “Wanatafuta Pepo.” Aseme: “Wamekwishaiona?” Waseme: “Hapana.” Aseme: “Vipi lau wangeiona?” Waseme: “Wangeiona basi wangelikuwa na bidii zaidi kulikoni.” Aseme: “Wanajilinda kutokamana na nini?” Waseme: “Wanajilinda kutokamana na Moto.” Aseme: “Kwani wamekwishauona?” Waseme: “Hapana.” Aseme: “Vipi wangeuona?” Waseme: “Wangeuona basi wangeukimbia na kujilinda nao zaidi kulikoni.” Ndipo aseme: “Mimi nakushuhudisheni kwamba nimewasamehe.” Waseme: “Wako ambao wameingia kimakosa. Wameingia humo kwa ajili tu ya haja.” Aseme: “Ni watu ambao matangamano yao si yenye kula khasara. Ni watu ambao matangamano yao si yenye kula khasara.”[1]
Ameipokea av al-Bukhaariy na Muslim.
[1] al-Bukhaariy (6408), Muslim (4689) na at-Tirmidhiy (3600).
Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk 90-91
Imechapishwa: 12/04/2024
taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/20-watu-ambao-matangamano-yao-si-yenye-kula-khasara/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)