Swali 20: Ni ipi hukumu ya mambo yanayofanywa na baadhi katika masherehe ya watu kupiga makofi na miluzi?
Jibu: Hukumu ya hayo ni kwamba yametoka kwa wasiokuwa waislamu. Kwa ajili hiyo haitakiwi kwa waislamu kuyafanya. Badala yake anatakiwa kusema “Allaahu Akbar” au “Subhaan Allaah” pindi jambo linapomfurahisha. Hata hivyo haya hayatakiwi kufanywa kwa pamoja, kama wanavofanya baadhi ya watu, bali mmojammoja. Kuhusu kusema “Allaahu Akbar” au “Subhaan Allaah” kwa njia ya pamoja wakati kunapotea kitu cha kufurahisha, ni jambo halina msingi wowote kutokana na ninavyojua.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: As-ilah Muhimmah, uk. 28
- Imechapishwa: 01/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)