Jina bora la Mitume ni la Nabii na Mtume wetu Muhammad bin ´Abdillaah. Swalah na salaam ziwe juu yake na ndugu zake wote katika Manabii na Mitume.
Baada ya wanachuoni kukubaliana juu ya kujuzu kuitwa kwa jina lake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wametofautiana juu ya hukumu ya kukusanya kati ya jina lake na kun-ya yake: Muhammad na Abul-Qaasim.
Ibn-ul-Qayyim (Rahimahu Allaah) amesema:
“Usawa ni kwamba inajuzu kuitwa kwa jina lake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), imekatazwa kuitwa kwa kun-ya yake. Baya zaidi ni kuitwa kwa majina yake yote mawili katika uhai wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Haijuzu kuitwa kwa jina lake na kun-ya yake yote mawili.”[1]
Hapa kunafuata faida ya kushangaza:
Mtu wa kwanza kuitwa Ahmad baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ilikuwa ni Ahmad al-Faraahiydiy al-Baswriy, baba wa al-Khaliyl. al-Khaliyl alizaliwa mwaka wa 100.
[1] Zaad-ul-Ma´aad (02/347).
- Muhusika: ´Allaamah Bakr bin ´Abdillaah Abu Zayd
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tasmiyat-ul-Mawluwd, uk. 18
- Imechapishwa: 18/03/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket