20. Hivi ndivo wanavoamini Mu´tazilah

Mu´tazilah. Wana ´Aqiydah moja na Qadariyyah na wana dini moja kama wao. Aidha wakapinga adhabu ya ndani ya kaburi, Uombezi na Hodhi. Hawaonelei kufaa kuswali wala swalah ya ijumaa nyuma ya muislamu yeyote isipokuwa yule ambaye ana mfano wa ´Aqiydah kama wao. Vilevile wanadai kuwa matendo ya waja hayakuandikwa kwenye Ubao uliohifadhiwa.

  • Mhusika: Imaam Harb bin Ismaa´iyl al-Kirmaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-us-Sunnah, uk. 79
  • Imechapishwa: 01/06/2022