Kwa kufupisha, huu ndio mpangilio wa ngazi nne za Qadar:
1 – Ujuzi wa Allaah kuyajua mambo kabla ya kuumbwa kwake.
2 – Kuyaandika mambo hayo.
3 – Kuyataka mambo.
4 – Kuyaumba.
Ni lazima pia mtu aamini kuwa yale aliyoyakosa hayakuwa yenye kumpata na yale yaliyompata hayakuwa ya kumkosa, kama ilivyopokelewa katika Hadiyth ya ´Ubaadah bin as-Swaamit katika wasia wake alipokuwa anamuuasia mwanae:
“Ee mwanangu kipenzi! Hakika hutopata ladha ya imani mpaka utambue kuwa yale yaliyokupata hayakuwa ya kukukosa na yale yaliyokukosa hayakuwa yenye kumpata.”[1]
[1] Abu Daawuud (4700).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Iymaan – Haqiyqatuhu wa Nawaaqidhwuh, uk. 27
- Imechapishwa: 01/05/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)