Allaah (Jalla wa ´Alaa) katika sifa Zake za kimatendo ni kwamba anazungumza. Kama ambavyo anaumba, anaruzuku, anahuisha na kufisha, anaendesha mambo, anapenda na kutaka (Subhaanahu wa Ta´ala) vilevile anazungumza maneno yanayolingana na utukufu Wake (Subhaanahu wa Ta´ala) kama zilivyo sifa Zake zingine. Anazungumza pindi anapotaka, anachokitaka na namna anayotaka.
Maneno ya Allaah aina yake ni ya kale milele (قديمة النوع), na yanazuka kutegemea na matukio (حادثة الآحاد). Kwa maana nyingine ni kwamba anazungumza anapotaka. Alizungumza kwa Qur-aan wakati wa kuteremka Kwake, anamzungumzisha Jibriyl, alimzungumzisha Muusa na Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) usiku alipandishwa mbingu. Kabla ya hapo alimzungumzisha Aadam (´alayhis-Salaam) na atazungumza siku ya Qiyaamah akiwafanyia watu hesabu. Atawazungumzisha waumini Peponi nao watamzungumzisha. Kwa hivyo anazumgumza kwa maneno maneno aina yake ni ya kale milele, na yanazuka kutegemea na matukio.
Vitabu vyote walivyoteremshiwa Mitume vyote ni maneno ya Allaah (Jalla wa ´Alaa). Miongoni mwavyo ni Qur-aan Tukufu ambayo ndio kubwa yavyo na Allaah amejaalia kuwa ndio yenye kuvihukumu. Kwa hivyo Qur-aan ni maneno Yake (Jalla wa ´Alaa) ya kikweli na sio mafumbo (مجازاً). Qur-aan imeteremka kutoka Kwake na haikuumbwa. Hii ndio ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Wanayasema haya kwa mdomo mpana.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh al-Mandhuumat-ul-Haaiyyah fiy ´Aqiydati Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 68
- Imechapishwa: 31/12/2023
Allaah (Jalla wa ´Alaa) katika sifa Zake za kimatendo ni kwamba anazungumza. Kama ambavyo anaumba, anaruzuku, anahuisha na kufisha, anaendesha mambo, anapenda na kutaka (Subhaanahu wa Ta´ala) vilevile anazungumza maneno yanayolingana na utukufu Wake (Subhaanahu wa Ta´ala) kama zilivyo sifa Zake zingine. Anazungumza pindi anapotaka, anachokitaka na namna anayotaka.
Maneno ya Allaah aina yake ni ya kale milele (قديمة النوع), na yanazuka kutegemea na matukio (حادثة الآحاد). Kwa maana nyingine ni kwamba anazungumza anapotaka. Alizungumza kwa Qur-aan wakati wa kuteremka Kwake, anamzungumzisha Jibriyl, alimzungumzisha Muusa na Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) usiku alipandishwa mbingu. Kabla ya hapo alimzungumzisha Aadam (´alayhis-Salaam) na atazungumza siku ya Qiyaamah akiwafanyia watu hesabu. Atawazungumzisha waumini Peponi nao watamzungumzisha. Kwa hivyo anazumgumza kwa maneno maneno aina yake ni ya kale milele, na yanazuka kutegemea na matukio.
Vitabu vyote walivyoteremshiwa Mitume vyote ni maneno ya Allaah (Jalla wa ´Alaa). Miongoni mwavyo ni Qur-aan Tukufu ambayo ndio kubwa yavyo na Allaah amejaalia kuwa ndio yenye kuvihukumu. Kwa hivyo Qur-aan ni maneno Yake (Jalla wa ´Alaa) ya kikweli na sio mafumbo (مجازاً). Qur-aan imeteremka kutoka Kwake na haikuumbwa. Hii ndio ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Wanayasema haya kwa mdomo mpana.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh al-Mandhuumat-ul-Haaiyyah fiy ´Aqiydati Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 68
Imechapishwa: 31/12/2023
https://firqatunnajia.com/17-vitabu-vyote-vya-mbinguni-ni-maneno-ya-allaah-na-hayakuumbwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)