113- Abud-Dardaa´ ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kambi ya waislamu siku ya Kichinjwa itakuwa al-Ghutwah karibu na mji wa Dameski ambao ndio mji bora wa Shaam.”[1]
Ameipokea Abu Daawuud, at-Twabaraaniy ameipokea kwa matamshi:
“Wakati huo ndio itakuwa sehemu bora ya kuishi… “
al-Haakim ameipokea kwa matamshi:
“Kipindi hicho ndiko itakuwa sehemu bora ya waislamu kuishi… “
Ibraahiym al-Junayd amesema:
“Nimemsikia Yahyaa bin Ma´iyn akiulizwa juu ya Hadiyth kuhusu kichinjwa cha rumi. Akasema: “Hakuna Hadiyth yoyote iliyopokelewa na watu wa Shaam ilio Swahiyh kama Hadiyth ya Swadaqah bin Khaalid.”
Bi maana Hadiyth ya Abud-Dardaa´ aliyopokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kambi ya waislamu siku ya Kichinjwa itakuwa al-Ghutwah karibu na mji wa Dameski ambao ndio mji bora wa Shaam.”
114- Ka´b-ul-Ahbaar amesema:
“Ngome ya waislamu wakati wa kichinjwa ni Dameski. Ngome yao dhidi ya ad-Dajjaal ni mto wa Jordan. Ngome yao dhidi ya Ya´juuj na Ma´juuj ni Twuur.”
115- al-Awzaa´iy amesema:
“Nimefikiwa na khabari ya kwamba Shaam kuna bonde linaloitwa al-Ghuutwah. Huko kuna mji unaoitwa Dameski na ndio itakuwa mji bora kabisa wa Shaam wakati wa Kichinjwa.”
116- ´Abdullaah bin Salaam amesema:
“Mwisho wa zama Dameski ndio itakuwa ngome ya waislamu kutokamana na Kichinjwa.”
117- ´Abdullaah bin ´Amr bin al-´Aasw akisema:
“Nakutamania kile ninachojitamania nafsi yangu na watoto wangu; Shikamana na Dameski.”
118- ´Abdullaah bin ´Amr bin al-´Aasw akisema:
“Sikupendelea kuishi Misri na hazini zake baada ya 150. Dameski ni bora lau wangelikuwa wanajua.”
119- Ibn Muhayriyz ameeleza kuwa Ruwayfiy´ bin Thaabit al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anh) – ambaye alimpa kiapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) chini ya mti – alimwambia:
“Ishi Palestina maadamu waarabu watakuwa wakingali wazuri. Pindi watapoanza kuita kama walivyokuwa wakifanya katika kipindi cha kishirikina basi hama kwenda Dameski – na mashariki yake ni bora kuliko sehemu zengine.”
120- Mak-huul amesema:
“Warumi watapora Shaam kwa masiku arubaini. Miji itayosalimika tu ni Dameski na ´Ammaan.”
121- Abul-A´yas ´Abdur-Rahmaan bin Salmaan amesema:
“Atakuja mfalme wa kigeni kutoka nje na atashinda juu ya miji yote isipokuwa tu Dameski.”
122- ´Abdus-Salaam at-Tanuukhiy amesema:
“Wanachuoni wetu wametueleza pindi walipoufungua mji wa Dameski wakati wa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) walipata jiwe lililokuwa limeandikwa kwa maandishi ya kigiriki. Hivyo wakamleta mwanamme wa kigiriki kulisoma. Kulikuwa yafuatayo:
“Dameski ni jabari. Hakuna jabari yeyote anayekusudia kuivamia isipokuwa Allaah humvunja. Majabari wanajenga na nyani zinaharibu. Hawa wa mwisho waliyotajwa ni waovu zaidi mpaka siku ya Qiyaamah.”
[1] Abu Daawuud (4298), Ahmad (57197), at-Twabaraaniy katika ”al-Awsat” (3205) na al-Haakim (4/486).
- Mhusika: Imaam ´Abdur-Rahmaan bin Rajab al-Baghdaadiy al-Hanbaliy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fadhwaa-il-ush-Shaam, uk. 127-136
- Imechapishwa: 10/02/2017
113- Abud-Dardaa´ ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kambi ya waislamu siku ya Kichinjwa itakuwa al-Ghutwah karibu na mji wa Dameski ambao ndio mji bora wa Shaam.”[1]
Ameipokea Abu Daawuud, at-Twabaraaniy ameipokea kwa matamshi:
“Wakati huo ndio itakuwa sehemu bora ya kuishi… “
al-Haakim ameipokea kwa matamshi:
“Kipindi hicho ndiko itakuwa sehemu bora ya waislamu kuishi… “
Ibraahiym al-Junayd amesema:
“Nimemsikia Yahyaa bin Ma´iyn akiulizwa juu ya Hadiyth kuhusu kichinjwa cha rumi. Akasema: “Hakuna Hadiyth yoyote iliyopokelewa na watu wa Shaam ilio Swahiyh kama Hadiyth ya Swadaqah bin Khaalid.”
Bi maana Hadiyth ya Abud-Dardaa´ aliyopokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kambi ya waislamu siku ya Kichinjwa itakuwa al-Ghutwah karibu na mji wa Dameski ambao ndio mji bora wa Shaam.”
114- Ka´b-ul-Ahbaar amesema:
“Ngome ya waislamu wakati wa kichinjwa ni Dameski. Ngome yao dhidi ya ad-Dajjaal ni mto wa Jordan. Ngome yao dhidi ya Ya´juuj na Ma´juuj ni Twuur.”
115- al-Awzaa´iy amesema:
“Nimefikiwa na khabari ya kwamba Shaam kuna bonde linaloitwa al-Ghuutwah. Huko kuna mji unaoitwa Dameski na ndio itakuwa mji bora kabisa wa Shaam wakati wa Kichinjwa.”
116- ´Abdullaah bin Salaam amesema:
“Mwisho wa zama Dameski ndio itakuwa ngome ya waislamu kutokamana na Kichinjwa.”
117- ´Abdullaah bin ´Amr bin al-´Aasw akisema:
“Nakutamania kile ninachojitamania nafsi yangu na watoto wangu; Shikamana na Dameski.”
118- ´Abdullaah bin ´Amr bin al-´Aasw akisema:
“Sikupendelea kuishi Misri na hazini zake baada ya 150. Dameski ni bora lau wangelikuwa wanajua.”
119- Ibn Muhayriyz ameeleza kuwa Ruwayfiy´ bin Thaabit al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anh) – ambaye alimpa kiapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) chini ya mti – alimwambia:
“Ishi Palestina maadamu waarabu watakuwa wakingali wazuri. Pindi watapoanza kuita kama walivyokuwa wakifanya katika kipindi cha kishirikina basi hama kwenda Dameski – na mashariki yake ni bora kuliko sehemu zengine.”
120- Mak-huul amesema:
“Warumi watapora Shaam kwa masiku arubaini. Miji itayosalimika tu ni Dameski na ´Ammaan.”
121- Abul-A´yas ´Abdur-Rahmaan bin Salmaan amesema:
“Atakuja mfalme wa kigeni kutoka nje na atashinda juu ya miji yote isipokuwa tu Dameski.”
122- ´Abdus-Salaam at-Tanuukhiy amesema:
“Wanachuoni wetu wametueleza pindi walipoufungua mji wa Dameski wakati wa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) walipata jiwe lililokuwa limeandikwa kwa maandishi ya kigiriki. Hivyo wakamleta mwanamme wa kigiriki kulisoma. Kulikuwa yafuatayo:
“Dameski ni jabari. Hakuna jabari yeyote anayekusudia kuivamia isipokuwa Allaah humvunja. Majabari wanajenga na nyani zinaharibu. Hawa wa mwisho waliyotajwa ni waovu zaidi mpaka siku ya Qiyaamah.”
[1] Abu Daawuud (4298), Ahmad (57197), at-Twabaraaniy katika ”al-Awsat” (3205) na al-Haakim (4/486).
Mhusika: Imaam ´Abdur-Rahmaan bin Rajab al-Baghdaadiy al-Hanbaliy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fadhwaa-il-ush-Shaam, uk. 127-136
Imechapishwa: 10/02/2017
https://firqatunnajia.com/16-ngome-ya-waislamu-kabla-ya-siku-ya-qiyaamah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)