Ahl-us-Sunnah wanaonelea kuwa Qur-aan ni maneno ya Allaah aliyozungumza. Kuna dalili tele zinazofahamisha kuwa Allaah anazungumza na kuita. Siku ya Qiyaamah Allaah atawaita waumini na makafiri:
وَيَوْمَ يُنَادِيهِمْ أَيْنَ شُرَكَائِي قَالُوا آذَنَّاكَ مَا مِنَّا مِن شَهِيدٍ
“Siku Atakayowaita: “Wako wapi [sasa] washirika Wangu?” Watasema: “Tunakiri Kwako hapana miongoni mwetu awezaye kushuhudia [hayo kuwa wapo].”[1]
وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰ أَنِ ائْتِ الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
“[Unakumbuka] pindi Mola wako alipomwita Muusa [na kumwambia]: “Nenda kwa watu madhalimu.”[2]
Katika Aayah nyingi Allaah ametukhabarisha kuwa alikuwa na mazungumzo ya manongonezo nae na vilevile akamwita. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَاللَّـهُ يَقُولُ الْحَقَّ وَهُوَ يَهْدِي السَّبِيلَ
“Allaah anasema ya haki Naye ndiye aongozaye njia [iliyonyooka].”[3]
Qur-aan inaeleza wazi kwamba Allaah anasema na kuzungumza na kwamba amezungumza kwa Qur-aah hii iliyoteremka kutoka Kwake:
تَنزِيلٌ مِّنْ حَكِيمٍ حَمِيدٍ
“[Hapana,] ni uteremsho kutoka kwa Mwenye hekima wa yote, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote.”[4]
Maneno haya asli yake ni yenye kutoka kwa Allaah (Tabaarak wa Ta´ala). Amemfunulia nayo Jibriyl na Jibriyl akamfikishia nayo Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ahl-ul-Ahwaa´ wana upotevu na kujigonga kunakopingana na Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amewawafikisha Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah haki na usawa katika mambo yote haya ambayo kuna maoni tofauti juu yake. Kwa kuwa wameshikamana na Kitabu cha Mola wao na Sunnah za Mtume wao (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wanaitakidi kuwa maneno ya Allaah ni haki na kwamba Allaah hasemi isipokuwa haki tu. Kusemwe nini sasa juu ya yule ambaye haonelei kuwa Qur-aan ni maneno ya Allaah na anaonelea kuwa imeumbwa?
[1] 41:47
[2] 26:10
[3] 33:04
[4] 41:42
- Muhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qurrat-ul-´Aynayn bi Tawdhwiyh Ma´aaniy ´Aqiydat-ir-Raaziyayn, uk. 23-24
- Imechapishwa: 15/10/2016
Ahl-us-Sunnah wanaonelea kuwa Qur-aan ni maneno ya Allaah aliyozungumza. Kuna dalili tele zinazofahamisha kuwa Allaah anazungumza na kuita. Siku ya Qiyaamah Allaah atawaita waumini na makafiri:
وَيَوْمَ يُنَادِيهِمْ أَيْنَ شُرَكَائِي قَالُوا آذَنَّاكَ مَا مِنَّا مِن شَهِيدٍ
“Siku Atakayowaita: “Wako wapi [sasa] washirika Wangu?” Watasema: “Tunakiri Kwako hapana miongoni mwetu awezaye kushuhudia [hayo kuwa wapo].”[1]
وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰ أَنِ ائْتِ الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
“[Unakumbuka] pindi Mola wako alipomwita Muusa [na kumwambia]: “Nenda kwa watu madhalimu.”[2]
Katika Aayah nyingi Allaah ametukhabarisha kuwa alikuwa na mazungumzo ya manongonezo nae na vilevile akamwita. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَاللَّـهُ يَقُولُ الْحَقَّ وَهُوَ يَهْدِي السَّبِيلَ
“Allaah anasema ya haki Naye ndiye aongozaye njia [iliyonyooka].”[3]
Qur-aan inaeleza wazi kwamba Allaah anasema na kuzungumza na kwamba amezungumza kwa Qur-aah hii iliyoteremka kutoka Kwake:
تَنزِيلٌ مِّنْ حَكِيمٍ حَمِيدٍ
“[Hapana,] ni uteremsho kutoka kwa Mwenye hekima wa yote, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote.”[4]
Maneno haya asli yake ni yenye kutoka kwa Allaah (Tabaarak wa Ta´ala). Amemfunulia nayo Jibriyl na Jibriyl akamfikishia nayo Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ahl-ul-Ahwaa´ wana upotevu na kujigonga kunakopingana na Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amewawafikisha Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah haki na usawa katika mambo yote haya ambayo kuna maoni tofauti juu yake. Kwa kuwa wameshikamana na Kitabu cha Mola wao na Sunnah za Mtume wao (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wanaitakidi kuwa maneno ya Allaah ni haki na kwamba Allaah hasemi isipokuwa haki tu. Kusemwe nini sasa juu ya yule ambaye haonelei kuwa Qur-aan ni maneno ya Allaah na anaonelea kuwa imeumbwa?
[1] 41:47
[2] 26:10
[3] 33:04
[4] 41:42
Muhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qurrat-ul-´Aynayn bi Tawdhwiyh Ma´aaniy ´Aqiydat-ir-Raaziyayn, uk. 23-24
Imechapishwa: 15/10/2016
https://firqatunnajia.com/13-qur-aan-kwa-mujibu-wa-ahl-us-sunnah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)